Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi
Seif Ali Iddi Kulia akionyeshwa moja ya aina ya vitakasa mikono vilivyotolewa
na Mfanyabiashara Mzalendo Nchini Mohamed Ibrahim Raza {Raza Lee} kusaidia
mapambano dhidi ya kuangamiza Virusi vya Corona Nchini.
Kati kati yao ni
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mheshimiwa
Mihayo Juma N’hunga
Mfanyabiashara Mohamed Ibrahim Raza akionyesha
Uzalendo wake wa kukubali kusaidia mchango wowote utaohitajika na Serikali
katika Ustawi wa Jamii Nchini
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa
Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Mihayo Juma N’hunga kati kati akizungumza na
Uongozi wa Taasisi ya Misaada ya Direct Aid na ule wa Manispaa ya Jiji la
Zanzibar uliofika Ofisini kwake kutoa Mchango wa kusaidia mapambano dhidi ya
Corona kwa niaba ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.
Naibu Waziri Mihayo Juma N’hunga akipokea
msaada wa vyakula tofauti kutoka kwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Misaada ya Direct
Aid Dr. Ayman Mohamed Jamal kwa kushirikiana na Uongozi wa Baraza la Manispaa
ya Jiji la Zanzibar.
Mheshimiwa Mihayo akimshukuru Mkurugenzi
wa Taasisi ya Misaada ya Direct Aid Dr. Ayman Mohamed Jamal mada baada ya
makabidhiwano ya mchango wa Vyakula kwa ajili ya Wananchi waliopata maambukizi
ya Corona.
Picha na – OMPR – ZNZ.
Na |Othman Khamis, OMPR
Wajumbe wa Kamati ya Wawakilishi wa Chama
cha Mapinduzi ya Baraza la Wawakilishi wameamua kutenga Shilingi Milioni
33,000,000/- bakaa ya Fedha za Mfuko wa Kamati hiyo zitakazotumika katika utengenezaji
wa Mask zitazosambazwa katika Majimbo yao ili kuwasaidia Wananchi kujikinga
dhidi ya Virusi vya Corona.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambae pia ni
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alitoa Taarifa hiyo Ofisini
kwake Vuga Mjini Zanzibar kufuatia kumalizika kwa Kikao chao cha kawaida
kilichopokea Taarifa ya Uwasilishwaji wa Mchango wao wa Shilingi Milioni
50,000,000/- zilizotolewa kuunga mkono nguvu
za Serikali katika mapambano dhidi ya Corona.
Balozi Seif Ali Iddi alisema Wajumbe hao
wameshateua Kamati itakayosimamia zoezi la utengenezaji wa Mask hizo kwa
kutumia Viwanda vya ndani kwani mbali ya kupunguza gharama kubwa ya uagizaji wa
vifaa hivyo kutoka nje ya nchi lakini pia mfumo huo wa kuwaamini wajasiri amali
wa Ndani utasaidia kuongeza mapato kwa Viwanda hivyo.
Alisema Kamati hiyo ya Wawakilishi wa CCM
ya Baraza la Wawakilishi bado ina jukumu la kuunga mkono kazi kubwa
inayoendelea kutekelezwa na Serikali Kuu katika kuangamiza Virusi vya Covid –
19 ambavyo ni janga la Dunia kwa wakati huu.
Balozi Seif akiwa Msimamizi Mkuu wa
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar aliwapongeza Wajumbe wa Kamati hiyo kwa
uamuzi wao huo wa busara utakaoleta faraja kwa Jamii kutokana na wazo
walilofikia la kutengeneza Vifaa vya
Kinga.
Mapema Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
Balozi Seif Ali Iddi akiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Kukabiliana na
Maafa Zanzibar alipokea msaada wa vifaa mbali mbali vilivyotolewa na
Mfanyabiashara Mzalendo Nchini Mohamed Ibrahim Raza { Raza Lee}kwa ajili ya
kusaidia nguvu za Serikali za kupambana na Corina.
Akipokea msaada huo uliojumuisha Sabuni,
Ndoo za Maji pamoja na vitakasa Mikono{
Sanitizer} zilizotengenezwa hapa Nchini Balozi Seif aliendelea kuwashukuru Wafanyabiashara,
Taasisi na Mashirika mbali mbali yaliyojitolea kuunga mkono jitihada za
Serikali.
Alisema Serikali Kuu inaendelea kujenga
matumaini kutokana na uelewa mkubwa wa baadhi ya Wananchi katika harakati zao
za kila siku huku wakiwa makini na janga la Corona licha ya baadhi ya Watu
kuendelea kukaidi baadhi ya maagizo yanayotolewa na Wataalamu wa Afya pamoja na
Viongozi wa Serikali.
Akikabidhi msaada huo wa vifaa
Mfanyabiashara Mohamed Ibrahim Raza {Raza Lee} alimuahidi Makamu wa Pili wa
Rais wa Zanzibar kwamba yuko tayari wakati wowote kutoa mchango wake pale
itakapohitajika kufanya hivyo.
Wakati huo huo Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alipokea mchango wa Tani 12 wenye Thamani ya Shilingi Milioni
21,000,000/- za Vyakula mbali mbali vilivyotolewa kwa pamoja kati ya Uongozi wa
Taasisi ya Misaada ya Direct Aid kwa
kushirikiana na Manispaa ya Jiji la Zanzibar.
Mchango huo wa Vyakula vitakavyosaidia
Wagonjwa wa Corona walihifadhiwa wa matibabu huko Kidimni na JKU Mtoni ulipokelewa
na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Mihayo
Juma N’hunga kwa niaba ya Balozi Seif ndani ya Jengo la Ofisi hiyo Vuga Mjini
Zanzibar.
Mh. Mihayo kwa niaba ya Balozi Seif alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
inaendelea kupata faraja na kujenga matumaini kutokana na Taasisi na Mashirika
tofauti ndani na nje ya Nchi kuendelea kuunga mkono jitihada za kupiga vita
Virusi vya Corona Nchini.
Alisema si vyema kwa Taasisi, mashirika na
Wadau wa misaada kama hivyo wakakata ghafla misaada yao wakati bado
haijaeleweka hadi sasa matatizo ya janga la Corona yanamalizika lini ambayo
mapambano yake yatawajibika kufanywa na kila Mtu hadi ukomo wake.
Wakitoa taarifa ya mchango huo Meya wa
Jiji la Zanzibar Mstahiki Saleh Juma Kinana na Mkurugenzi wa Taasisi ya Misaada
ya Direct Aid Dr. Ayman Mohamed Jamal kwa pamoja walisema msaada huo ni
muendelezo wa Ushirikiano uliopo kati ya Taasisi hizo na Serikali Kuu.
Walisema wao kama Viongozi wa Taasisi zao
watajitahidi katika kuona yale malengo yao ya kusaidia ustawi na Maendeleo ya
Umma unafika na kumgusa kila Mwananchi ndani ya Taifa hili.
Vyakula vilivyotolewa na kukabilidha kwa
Kamati ya Kukabiliana na Maafa kwa pamoja kati ya Uongozi wa Baraza la Manispaa
ya Jiji la Zanzibar na Taasisi ya Misaada ya Direct Aid ni pamoja na Mchele,
maharagwe, Mafuta ya Kupikia, Unga wa Ngano pamoja na Sukari.
No comments:
Post a Comment