Kamishna
wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Dkt. Fatma Rashid Khalfani
(kushoto) akikabidhi zawadi ya Keki kwa Mkurugenzi wa Wauguzi wa Hospitali ya
Mkoa wa Dodoma, Stanley Mahundo (kulia) ikiwa ni ishara ya kuwapongeza Wauguzi
kwa kazi nzuri wanayoifanya. Pamoja na keki hiyo, Dkt. Fatma alikabidhi pia
sabuni kwa ajili ya Wauguzi hao kuzitumia kunawia mikono kwa ajili ya kujikinga
na Korona.
Kamishna
wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Dkt. Fatma Rashid Khalfani
(Kulia) akiongea na Mkurugenzi wa Wauguzi katika Hospitali ya Mkoa Dodoma,
Stanley Mahundo alipomtembelea Hospitali hiyo kwa lengo la kuwapongeza Wauguzi
kuelekea maadhimisho ya Siku ya wauguzi duniani inayosheherekewa Mei 12 ya kila Mwaka.
Sister
Fidence, MC, Mkuu wa Kituo cha kutunza
Watoto na Wazee cha Home of Joy and Love
Kilichopo Hombolo jijini Dodoma akimtembeza Kamishna wa Tume ya Haki za
Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Dkt. Fatma Rashid Khalfani (kulia) kumuonesha
maeneo mbalimbali ya kituo hicho Mei 11, 2020. Ziara hiyo ya Kamishna ilikuwa
na lengo la kutoa elimu ya haki ya afya ili kuwahamasisha kuendelea kuzingatia
maelekezo yanayotolewa ya kujikinga na maradhi ya Korona. Kushoto ni Afisa wa
THBUB, Fides Shayo.
Mkuu
wa Kituo cha kutunza Watoto na Wazee cha
Home of Joy and Love kilichopo
Hombolo, Dodoma, Sister Fidence MC (kulia) akimuonesha Kamishna wa Tume ya Haki
za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Dkt. Fatma Rashid Khalfani (katikati)
mabweni wanayokaa Watoto alipotembelea
kituo hicho Mei 11, 2020. Kushoto ni Afisa wa THBUB, Fides Shayo.
No comments:
Post a Comment