Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein akitowa heshima kwa mwili wa Marehemu Balozi Mstaaf Job Lusinde alipofika nyumbani kwa marehemu mtaa wa uzunguni jijini Dodoma kwa kutowa mkuno wa pole kwa Wanafamilia ya marehemu leo kulia Waziri Mkuu Mstaaf wa Tanzania Ndugu wa marehemu Mhe. John Malecela
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akisaini kitabu cha maombolezi ya Marehemu Balozi Mstaaf Mhe.Job Lusinde alipofika nyumbani kwa marehemu mtaa wa Uzunguni Jijini Dodoma leo, kutowa mkono wa pole kwa Wanafamilia ya marehemu.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimfariji Mke wa Marehemu Balozi Mstaaf Job Lusinde alipofika nyumbani kwaom leo kutowa mkono wa pole kwa Wanafafilia.
RAIS wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, ametoa mkono wa
pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wa Marehemu Balozi Mstaafu Job
Malecela Lusinde aliyefariki dunia alfajiri ya Jumanne Julai 7, 2020.
Rais Dk. Shein alifika nyumbani kwa marehemu Balozi Mstaafu
Job Lusinde majira ya asubuhi huko katika Mtaa wa Uzunguni Jijini Dodoma mbapo
alitoa mkono wa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki ikiwani pamoja na
kumpampole Mjane wa Marehemu Sara Lusinde.
Akitoa mkono wake wa pole Rais Dk. Shein alieleza jinsi
alivyoguswa na kifo cha aliyekuwa miongoni mwa Mawaziri 11 wa Kwanza wa
Tanganyika ambapo alieleza kuwa kiongozi huyo Mkongwe wa siasa atakumbukwa kwa
mchango wake mkubwa akiwa Waziri, Balozi, Mdhamini wa CCM na kiongozi wa Wazee
wa Dodoma.
Aidha, Rais Dk. Shein alipata fursa ya kuuaga mwili wa Marehemu Balozi
Lusinde akiwa pamoja na ndugu, jamaa, marafiki pamoja na viongozi mbali mbali hapo
nyumbani kwake mtaa wa Uzunguni Mjini Dodoma.
Mapema Rais Dk. Shein alipofika nyumbani kwa Marehemu alitia saini kitabu
cha maombolezi ambapo alitoa pole kwa kifo cha Mzee Balozi Job Lusinde kwa
wafiwa wote, ndugu na jamaa huku akimuomba
Mwenyezi Mungu awape subira na aiweke roho ya Marehemu pahala pema.
Akitoa neno la shukurani kwa Rais Dk. Shein Waziri Mkuu Mstaafu John
Samweli Malecela alimshukuru na kumpongeza Rais Dk. Shein kwa kushiriki
kikamilifu katika msiba huo na hatimae kuuaga mwili wa marehemu.
Mwanasiasa
huyo mkongwe, Balozi Job Lusinde (90)
alikuwa mmoja wa viongozi katika Baraza la Kwanza la Mawaziri la Mwalimu Julius
Nyerere baada ya uhuru ambaye alifariki dunia katika Hospitali ya Mloganzila
jijini Dar es Salaam.
Familia ya Balozi Lusinde na Malecela ilieleza kuwa
taratibu za mazishi zinaendelea asubuhi hii na baadae mwili wa marehemu
utapelekwa katika Kanisani kwa ajili ya kuendelea na taratibu nyengine za mazishi.
Marehemu Lusinde ni kaka wa Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania, John Samweli Malecela.
Marehemu Balozi Lusinde amezaliwa Oktoba 9, 1930 na
aliwahi kuwa Waziri wa Mawasiliano mwaka 1965 na ni miongoni mwa watu
waliofanya kazi kwa ukaribu na Mwalimu Julius Nyerere kama Waziri wa Serikali
za Mitaa mwaka 1961.
Pia, aliwahi kuwa Balozi wa Tanzania nchini China
kuanzia mwaka 1975 hadi mwaka 1984 pamoja na kuwa Balozi wa Tanzania nchini
Kenya.
Aidha, Marehemu Balozi Lusinde ndio kiongozi pekee aliyekuwa
amebaki hai akiwa miongoni mwa Mawaziri wa Baraza la Kwanza la Mawaziri wa
Serikali ya Awamu ya Kwanza iliyoongozwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage
Nyerere.
Mwili wa kiongozi huyo unatarajiwa kuzikwa leo katika
makaburi ya Kikuyu jirani na Chuo Kikuu cha Mtakatifu Yohana Jijini Dodoma.
Mara baada ya kutoa mkono wa pole Rais Dk. Shein ambaye
pia, ni Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar alielekea katika Ukumbi wa Kituo cha
Mikutano cha Jakaya Kikwete Jijini Dodoma kushiriki kikao cha Halmashauri Kuu
ya CCM (NEC).
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment