kuwa kuanzia leo Julai 29, 2020 Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam utaitwa
Uwanja wa
Uwanja wa Benjamin Mkapa (Benjamin Mkapa Stadium) ili
kuendelea kumuenzi Rais huyo wa
awamu ya Tatu.
Rais Magufuli ametoa tamko hilo katika hafla ya kuaga mwili wa aliyekuwa
rais wa serikali ya
awamu ya tatu Hayati
Benjamin William Mkapa iliyofanyika katika Uwanja wa Uhuru
Dar es Salaam ambapo
alisisitiza Mzee Mkapa alikuwa na
mchango mkubwa katika sekta ya
michezo nchini hivyo taifa tunapaswa kumuenzi .
“Mzee Mkapa aliujenga uwanja mkubwa wa michezo na alikua
hapendi vitu viitwe kwa jina
lake,lakini kwakuwa kwa sasa amelala na hawezi kuniadhibu na
kwakua nimepokea meseji
nyingi nimekubali na sasa natamka rasmi uwanja ule uitwe Mkapa
Stadium,”Dkt.Magufuli.
Dkt.Magufuli ameongeza katika Michezo Mzee Mkapa alikuwa anapenda sana
michezo ndio
maana amefanya mambo mengi sana katika sekta hiyo,vile vile
alikua ni Shabiki wa Timu ya
Yanga japo hakuwahi
kuonyesha hadharani hivyo tunapaswa kumkumbuka na kutunza
kumbukumbu hizo.
Hata hivyo Uwanja wa Taifa Dar es Salaam (Mkapa Stadium) ni
miongoni mwa viwanja
vikubwa barani Afrika ambavyo vimekidhi vigezo vyote
vilivyoanishwa na Shirikisho la
Soka Duniani FIFA na una uwezo wa kuingiza mmashabiki takriban
elfu sitini.
Hivi karibuni watu wengi walionyesha nia yao ya kuomba uwanja
huo uitwe jina la
Mzee Mkapa kama njia ya kumuenzi Rais huyo mstaafu ambayo leo
Mhe.Rais ameitimiza nia hiyo.
Pamoja Mheshimiwa Rais Magufuli aliendelea kusisitiza kuwa Mzee
Mkapa katika sekta ya Sanaa
napo ameacha alama
kwani ndiye aliyeanzisha Chama cha Hakimiliki na Hakishiriki (COSOTA)
ambayo kwa sasa ni taasisi rasmi lengo ni kuwasaidia wasanii
kupata haki za kazi zao na
katika sekta ya Habari
ndiye muasisi wa Vitengo vya Habari na Mawasiliano katika wizara.
Naye mmoja wa wananchi na shabiki wa mpira nchini Bw.Athuman
Ugassa amepongeza uamuzi
Mheshimiwa Rais Magufuli wa kuupa uwanja huo jina lake kwani
uwanja huo ni alama ya
mchango wake katika kuendeleza sekta ya michezo nchini.
|
MICHANGO ISIZUIE MTOTO KUPATA ELIMU
-
Na Angela Msimbira, NZEGA
NAIBU Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe.
Zainab Katimba amesisitiza kuwa uchangiaji katika sekta ya...
5 hours ago
No comments:
Post a Comment