Habari za Punde

Uzinduzi wa Mkutano wa Kampeni Jimbo la Kwahani Zanzibar

Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali Maulid akimnadi Mgombea wa Ubunge wa Jimbo la Kwahani Ahmed Yahya Abdul-wakil  huko katika uwanja wa Jimbo la Kwahani Zanzibar 
Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali Maulid akimnadi  Mgombea uwakilishi wa jimbo la kwahani Yahya Abdalla Rashid huko katika uwanja wa Jimbo la Kwahani Zanzibar 
Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali Maulid akimnadi Diwani wa Wadi ya Muungano, Mahmoud Ali  Makame  huko katika uwanja wa Jimbo la Kwahani Zanzibar.
 Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kwahani  Ahmed Yahya Abdul-wakil akiomba kura na kunadi sera zake kwa Wananchi wa Jimbo la Kwahani (hawapo pichani)  huko katika uwanja wa Jimbo la Kwahani Zanzibar ,   

 Baadhi ya wanachama wa chama cha mapinduzi wakisikiliza sera za mgombea uwakilishi kwa jimbo la kwahani Yahya Abdalla  Rashid (hayupo pichani ) huko katika Uwanja wa Jimbo la Kwahani Zanzibar .

Picha na Khadija Khamis - Maelezo Zanzibar.

Na.Sabaha Khamis - Maelezo Zanzibar.                                                                                                      

Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali Maulid amewataka wanachama wa Chama cha Mapinduzi kukipigia kura Chama hicho ili kuendelea kuwaletea maendeleo nchini.

Amesema hayo wakati wa kuwatambulisha wagombea wa Ubunge, Uwakilishi na Udiwani wa Jimbo la Kwahani katika  uzinduzi wa Kampeni iliyofanyika  uwanja wa branch ya Kwahani.

Amesema wananchi wasipoteze kura zao kwa kuwapigia  wagombea wasiowakweli  na badala yake wawachaguwe  wagombea wa Chama Cha Mapinduzi ambao  sera zao ni zakuleta maendeleo.

Ameeleza kuwa Jimbo la Kwahani ni Jimbo lakupigiwa mfano kwani ni Jimbo lilitoa Mgombea Urais wa Zanzibar kwa Chama cha Mapinduzi.

Hata hivyo amewaomba kuwapigia kura Mgombea wa Urais wa Jamuhuri ya Muungani wa Tanzania Dk. John Joseph Magufuli, Mgombea Mwenza Mama Samia Suluhu Hassan,  Mgombea wa Urais wa Zanzibar Dk. Hussein Mwinyi pamoja na Wabunge,,Wawakilishi na Madiwani kupitia chama hicho .

Nae Mgombea Ubunge  Jimbo hilo Ahmed Yahya Abdul-wakil amewataka wanachama wa Jimbo la Kwahani kumpigia kura na kumpa ushindi wa kishindo kwani kufanya hivyo nikukipa nguvu chama hicho ili kiendelee kushika dola .

Ameahidi kuvaa viatu vya Dk. Mwinyi ili kuleta maendeleo katika Jimbo hilo, kuimarisha vikundi vya Wajasiriamali kwa  kuwapatia mitaji,  kuwatafutia kituo cha kisasa kuweza kuuza bidhaa zao,kuwaendeleza wasanii na michezo ndani na nje ya nchi.

Pia Mgombea Uwakilishi wa Jimbo la Kwahani amesema iwapo atapewa ridhaa ya kuongoza katika Jimbo atashirikiana na Wagombea wenzake kuimarisha maendeleo ya Jimbo hilo.

Pamoja na hayo baadhi ya Wagombea ambao kura zao hazikutosha wameahidi kushirikiana na walioteuliwa ili kuhakikisha wanakipatia ushindi chama hicho katika uchaguzi mkuu 28 Okt 2020.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.