Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akiwataka viongozi wote wa Vyama na Mashirikisho ya Michezo kuhakikisha kila mmoja anawajibika katika kutoa maoni, alipokuwa akifungua Warsha ya kutoa maoni katika Rasimu ya Kanuni zitakazoasiliwa kwa ajili ya kupinga mbinu haramu za matumizi ya madawa za kusisimua misuli na kuongeza nguvu michezoni (Anti Doping) iliyofanyika Novemba 19, 2020 Jijini Dar es Salaam, (katikati) Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Yusuph Singo.
Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Yusuph Singo akiwasihi Wadau wa Michezo kulichukulia kwa uzito suala la Anti Doping na kuharakisha utoaji maoni, ili kuepusha taifa kufungiwa ushiriki wa michezo ya Kimataifa, Novemba 19, 2020, Jijini Dar es Salaam, katika ufunguzi wa Warsha ya kutoa maoni ya rasimu ya kanuni zitakazo asiliwa za kupinga mbinu haramu za matumizi ya dawa za kusisimua misuli na kuongeza nguvu michezoni.
Wadau wa Michezo
wakifuatilia Warsha ya kutoa maoni ya Rasimu ya Kanuni zitakazoasiliwa za
kupinga mbinu haramu za matumizi ya dawa za kusisimua misuli na kuongeza nguvu
michezoni iliyofanyika leo Novemba 19, 2020 Jijini Dar es Salaam.
Na Anitha Jonas – WHUSM, Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan
Abbasi amewataka viongozi wa Mashirikisho na Vyama vya Michezo kuwa wabunifu na
kuandaa mikakati ya kukuza na kuendeleza michezo nchini.
Dkt. Abbasi ametoa
kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akifungua Warsha ya Wadau wa Michezo
nchini ya kutoa maoni ya katika rasimu
ya Kanuni za Taifa za Kupinga mbinu haramu na matumizi ya dawa za kusisimua
misuli na kuongeza nguvu michezoni (Anti
Doping).
Akizungumza katika Warsha
hiyo Katibu Mkuu huyo na Msemaji Mkuu wa Serikali alisisitiza kuwa kila kiongozi wa Chama na Mashirikisho
ya Michezo atimize wajibu wake kwa kutoa maoni ili kujiepusha na kero ya
wanamichezo kuja kufungiwa kushiriki michezo na kuliletea taifa aibu.
“Najua mnafahamu kuwa
taasisi hii ya kupinga matumizi ya mbinu haramu na dawa za kuongeza nguvu
michezoni namna ilivyo na nguvu hivyo ni vyema suala hili mkalifanya kwa umakini, ili kuiepusha nchi
kuwekewa vikwazo vya kushiriki michezo mbalimbali kimataifa,” alisema Dkt.Abbasi.
Kwa upande wa
Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo Michezo Tanzania Bw.Yusuph Singo alisema
Kamati ya Anti Doping kwa sasa imefanya kazi ya kuandaa kanuni ambazo zitakazo
asiliwa na kuwa za kitaifa na badae serikali itaunda sheria ya kusimamia
masuala hayo ya kupinga mbinu haramu michezoni.
“Kenya
walisitishiwa kushiriki mashindano ya
Kimataifa kwa kukosa “codes” ambazo zinaendana na mazingira ya nchi yao, ambazo
ndiyo hizi kanuni tulizoandaa hivyo, ningependa suala hili tulichulie uzito na
tulikamilishe haraka ili kuepusha taifa na chagamoto kama hii na tungependa
kanuni hizi zianze kutumika mapema mwakani,” alisema Bw.Singo.
Halikadhalika nae
Katibu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania Bw.Philbert Bayi aliishukuru Serikali kwa
kufanikisha kusainiwa kwa mkataba huo wa kupinga matumizi ya mbinu haramu
michezoni mnamo mwaka 2017, kwani
Tanzania ilikuwa ni moja ya nchi chache zilizokuwa bado hazijasaini mkataba
huo.
No comments:
Post a Comment