STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE
OF THE PRESS SECRETARY
PRESS
RELEASE
Zanzibar Disemba 10, 2020
RAIS
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhadj Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema
Viongozi wa kisiasa wana dhima kubwa mbele Mwenyezi Mungu na kubainisha maridhiano ya
kisiasa yaliofanyika yameonyesha njia sahihi katika kudumisha umoja na
mshikamano nchini.
Alhadj
Dk. Mwinyi amesema hayo katika Dua maalum ya kuiombea nchi na viongozi wake
amani, hafla iliyofanyika katika
Msikiti wa Mushawarra uliopo Muembeshauri
Jijini hapa.
Alisema
kuna umuhimu kwa wananchi kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwaongezea neema ya
maridhiano yaliofanikisha uundaji wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, baada ya
uchaguzi mkuu kumalizika.
Alisema
viongozi wana dhima kubwa ya kuhakikisha wanadumisha amani na mshikamano na
hivyo akatumia fursa hiyo kumpongeza Makamo wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif
Sharrif Hamad na Chama chake cha ACT Wazalendo kwa kukubali kushiriki katika Serikali
ya Umoja wa Kitaifa (SUK).
Alisema
yeye binafsi anaamini Wazanzibari wote ni kitu kimoja wakiwa na dhamira ya
kuijenga Zanzibar na hivyo akawataka viongozi wa Dini kuendelea kuwaombea dua
viongozi ili waendelee kuiongoza nchi kwa ufanisi.
“Viongozi wana dhima kubwa kwa Mwenyezi Mungu
…..maridhiano yaliofanyika yameonyesha mwelekeo sahihi wa nchi“
Alieleza
kuwa pamoja na Wazanzibari kuwa na mengi ya kumshukuru Mwenyezi Mungu, pia
wanapaswa kuendeleza amani iliopo nchini ili kazi ya kuleta maendeleo na kukuza
uchumi wa Taifa iweze kufanikiwa.
Alhadj
Dk. Mwinyi alisema wakati wa kampeni za Uchaguzi mkuu uliopita alitowa ahadi
nyingi sana kwa wananchi ikiwemo ile ya
kusisitiza kuendeleza amani na utulivu
iliopo nchini pamoja na kuwataka wananchi kuunga mkono juhudi za
Serikali katika kufanikisha azma hiyo.
Aidha,
aliwataka Wazanzibari kufanya kazi kwa
bidii kwa kila mmoja kutekeleza wajibu wake kikamilifu mahala alipo ili kuleta
ustawi wa maisha ya wananchi.
Alitoa
shukurani kwa wananchi wote wa Zanzibar kwa hatua zao za kumtumia pongezi kwa
kuleta maridhiano na kubainisha kuwa hatua hiyo
inaleta matumaini kuwa wananchi wengi wameridhia na kukubali jambo hilo.
Vile
vile alisiitiza dhamira yake ya kuendelea kusimamia Umoja na mshikamano katika
nchini ili kuharakisha kasi ya maendeleo.
Alhadj
Dk. Mwinyi alimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuendelea kuibariki Zanzibar na kubaki katika hali ya mani, sambamba na
kuwapongeza waandaaji wa Dua hiyo kwa kuona umuhimu wa kumshukuru Mwenyezi
Mungu kwa kupokea maombi yao , ikizingatiwa dua kama hiyo ilifanyika kabla ya
Uchaguzi mkuu wa Oktoba 25, 2020.
Mapema,
Waziri wa Nchi (OR) Katiba, sheria,Utumishi wa Umma na Utawala Bora Haroun Ali
Suleiman alitoa shukran kwa viongozi wakuu wa Kitaifa pamoja na wananchi
waliohudhuria katika hafla hiyo muhimu yenye faida kubwa kwa taifa.
Nae,
Katibu wa Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khalid Mfaume
alisema dua hiyo inalenga kumshukuru Mwenyezi Mungu pamoja na kumuombea
Dua Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhadj Dk. Hussein
Ali Mwinyi na wasaidizi wake ili waweze kutekeleza vyema majukumu yao ya
kitaifa.
Viongozi
mbali mbali wa kitaifa walihudhuria katika dua hiyo wakiwemo Marais Wastaafu
Alhadj Amani Abeid Karume, Alhadj Ali Mohamed Shein, Alhadj Balozi Seif Ali
Idd, Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariamu Ali Mwinyi, Katibu wa Baraza la
Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, Mufti Mkuu wa
Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kaabi, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Dk. Mwinyi Talib
Haji, Mawaziri, Mwakilishi wa Mufti Mkuu
kutoka Tanzania Bara Sheikh Alhad Mussa
Salum pamoja na wananchi wa Mikoa ya Unguja.
Abdi
Shamna, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422
Tel.:0777476982. Fax: 024 2231822
E-mail: abdya062@gmail.com
No comments:
Post a Comment