Habari za Punde

Taasisi ya Elimu kuiboresha mitaala kwa ajili ya ustawi wa Taifa

 Na Maulid Yussuf WEMA


Taasisi ya Elimu ya Zanzibar inaendelea kupitia vyema mtaala wa elimu ya maandalizi na msingi  ili Taifa lipate  Elimu bora.

Hayo yameelezwa na  Meneja wa  mtaala na vifaa kutoka Taasisi ya elimu  ya Zanzibar  mwalimu Abdallah Mohamed Mussa,  wakati akifungua kikao cha siku moja  kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo katika ukumbi wa ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Mazizini mjini Unguja.

 Amesema upitiaji wa Mtaala ni Safari ndefu kwani ilianza tokea  January 2019 kwa kukusanya maoni kutoka kwa wadau mbali mbali kwa ajili ya kutoa maoni yao  ili kupata mtaala ulio bora katika nchi.

Amesema katika kufanikisha hilo  Taasisi imefanikiwa kupitia mitaala ya nchi 12 ili kulingalisha na kupata uzoefu katika masuala ambayo mtaala wa Zanzibar hayamo kwa lengo la kuimarisha na kupata mtaala bora kwa wanafunzi.

Amefahamisha kuwa katika mtaala huo mpya baada ya kukamilika wana mategemeo makubwa kuwa watoto watakaomaliza Elimu ya maandalizi wataweza kujua kusoma, kuandika na kuhesabu pamoja na kuwa na ubunifu kwa mujibu wa daraja lake la elimu ambao utaweza kumjenga kadri anavyokuwa na kuweza kujiajiri hapo baadae.

Amesema kikao hicho ni kina lengo la kupitia mawanda na mtiririko mtaala ya Skuli za maandalizi, hivyo amewataka kuitumia nafasi hiyo na kushauri kutoa maoni  kwa kuwaangalia zaidi watoto wetu ili kupata elimu bora nchini.


Nae msaidizi wa kituo cha Taifa cha Walimu NTRC mwalimu Mohammed Khamis Suleiman amesema upitiaji wa mtaala ni jambo muhimu sana na Taasisi ya Elimu imeamua kuweka makundi mbalimbali kwa lengo la kutoa maoni yao juu ya mawanda hayo ili kuweza kufikia malengo ya nchi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.