Habari za Punde

Uzinduzi wa Kampeni Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Muhambwe Mkoani Kigoma.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Kassim Majaliwa akimsikiliza  Kada wa CCM, Jamal Tamimu (katikati) alipomuombea kura  mgombea wa CCM  Dkt Florence Samizi  (kulia) katika Uchaguzi Mdogo  kwenye Jimbo  la Muhambwe Mkoani Kigoma, katika  uzinduzi wa kampeni za CCM uliofanyika kwenye uwanja wa Taifa wa Kibondo, Mei 4, 2021. Tamimu alikuwa ni mmoja wa WanaCCM wenye ushawishi mkubwa walioshiriki katika kura za maoni kuwania uteuzi wa Chama chao. 
Kada wa CCM, Jamal Tamimu  akimuombea kura mgombea Ubunge kwa tiketi ya CCM katika uchaguzi mdogo kwenye  Jimbo la Muhambwe Mkoani Kigoma wakati Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Kassim Majaliwa  alipozindua kampeni hizo kwenye uwanja wa Taifa wa Kibondo, Mei 4, 2021. Jamal alikuwa ni mmoja wa wagombea wenye ushawishi mkubwa katika kura za maoni za wana CCM waliowania uteuzi wa kupeperusha bendera ya Chama chao kwenye Jimbo hilo
 Mmoja kati  wanachi  wengi wa Kibondo waliojitokeza kumsikiliza Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Kassim Majaliwa wakati alipozindua kampeni za CCM katika  uchaguzi mdogo wa Jimbo la Muhambwe Mkoani Kigoma kwenye Uwanja wa Taifa wa Kibondo, Mei 4, 2021. Dkt. Florence Samizi ndiye mgombea wa CCM katika jimbo hilo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.