Habari za Punde

Kamati ya Bajeti BLW yaishauri Wakala wa Serikali Mtandao Zanzibar kufanya kazi kwa bidii

Wajumbe wa kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi chini ya mwenyekiti wake Mhe Ali Suleiman Ameir wakitoa ushauri kwa watendaji wa wakala wa Serikali mtandao Zanzibar wakati walipofika ofisini kwa ajili ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa majukumu yao kwa kipindi cha julai 2020 - juni 2021.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi Mhe Ali Suleiman Ameir akisikiliza changamoto na mafaniko ya watendaji wa wakala wa serikali mtandao katika kutekeleza majukumu yao.


 Na Mwandishi wetu

Kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi imeishaurI Wakala wa Serikali Mtandao Zanzibar (eGAZ) kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuweza kufikia azma ya kuwa kitovu cha utaalamu na ubunifu katika kuandaa sera, viwango na taratibu nyengine kwa ajili ya kuimarisha matumizi ya tehama nchini.

 

Wajumbe wa Kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake Mhe Ali Suleiman Ameir wametoa ushauri huo mara baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa wakala wa serikali mtandao kwa kipindi cha julai 2020 – juni 2021 katika kikao kilichofanyika katika ofisi ya wakala hio huko Mazizini.

 

Wamesema Serikali pamoja na wananchi wanaitegemea sana wakala hio kutokana na umuhimu wake mkubwa katika mapinduzi ya matumizi ya teknolojia ambapo ni wajibu kuhakikisha mifumo yao wanaiimarisha na kuiendeleza kwa mujibu wa sera, viwango pamoja na kutumia mifumo sahihi ya tehama kwa urahisi nchi nzima .

 

Mapema Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Serikali Mtandao Zanzibar,  Said Seif Said akiwasilisha taarifa ya utekelezaji kwa kipindi cha  julai 2020 –juni 2021 ameielezea kamati hiyo kwamba  serikali mtandao ina fursa kubwa ya kuleta mabadiliko katika utendaji wa kazi serikalini na kutoa huduma bora pamoja na kuongeza wingi wa ukusanyaji wa mapato.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.