Mkurugenzi Mipango Sera na Utafitii Bi Daima M. Mkalimoto akifungua mafunzo kwa maafisa Tehama na wakuu wa vitengo wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais
Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya matumizi ya Tehama wakisikilliza kwa makini wakati mafunzo yakiendelea.
Na Raya Hamad – OMKR.
Maafisa Tehama na wakuu wa vitengo wametakiwa kuwa wabunifu na kushirikiana
katika majukumu yao ya kazi ili kuendana na kasi ya iliyopo ya ukuwaji wa
teknologia ulimwenguni
Mkurugenzi Mipango, sera na utafiti Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais
Zanzibar Bi Daima Mohammed Mkalimoto ameyasema hayo leo wakati akizindua
mafunzo kwa maofisa tehama na wakuu wa vitengo wa ofisi hio na taasisi
zilizochini yake kwenye ukumbi wa mkutano wa ofisi hio Migombani.
Amesema serikali mtandao inatakiwa kuwa hai muda wote katika kutoa
ushirikiano ili iwe ni suluhisho la kiutendaji katika mabadiliko na kufanya
masuala ya tehama kuwa rahisi na kuwa na mfumo mmoja wenye tija kwa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar .
Nae mkufunzi wa mafunzo hayo Ndugu Ali Abdi Ali kutoka Serikali Mtandao
amesema maafisa tehama ili waendane kasi ya mabadiliko ya mawasiliano ni muhimu
wawe wanapatiwa mafunzo ya mara kwa mara
jambo ambalo litapelekea kuwa umakini katika utendaji wao wa kazi.
Aidha washiriki wa mafunzo hayo waishukuru Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa
Rais na kuomba muendelezo wa mafunzo hayo ili kuwa weledi zaidi na kufahamu
maendeleo ya mawasiliano ya tehama.
No comments:
Post a Comment