Na Mwashungi Tahir Maelezo 29-9-2021.
Mwenyekiti wa Kamati tekelezaji
ya UWT Wilaya ya Amani Fatma Amrani Abdullah amewataka viongozi wa Chama Cha Mapinduzi na jumuiya
kushirikiana kuwa karibu na
wanachama wao ili waweze kusikiliza changamoto zinazowakabili ili wakae pamoja
na kuzitatua.
Ameyasema hayo leo huko Wilaya ya Amani wakati kamati tekelezaji ya
UWT Wilaya Amani ilipokuwa na ziara ya kuwakagua waasisi wa UWT ambao hivi sasa
wagonjwa ikiwa ni miongoni mwa maadhimisho ya wiki ya UWT ambayo inatarajiwa
kuadhimishwa ifikapo tarehe 4-10-2021.
Amesema ni faraja kubwa kuwatembelea akinamama hao ambao
wametumikia Chama na Jumuiya zake kwa muda mrefu na kufikia pahala pazuri
katika utendaji na kuwaomba viongozi wa
ngazi zote ikiwemo Mkoa na Wilaya na
viti maalum wa UWT kuwapitia mara kwa mara
na kuwafariji ili waone mchango wao unatambulika kwa kipindi chote
walichotumikia .
“Nawaomba viongozi wenzangu tuwe na muda wa kuwatembelea
wanachama wenzetu huku tukikumbuka mchango wao waliofanya katika chama na
jumuiya itawapelekea kuhamasika na kujua na wao wanakumbukwa kwa yale waliyofanya katika kuleta
maendeleo katika majimbo yao”, alisema
Mwenyekiti huyo.
Aidha amesema akinamama hao walikuwa mstari wa mbele katika
kukiendeleza chama pamoja na jumuiya kwa kuleta maendeleo katika mambo mbali
mbali kuhakikisha jumuiya inasonga mbele
kwa kupatikana viongozi waliyo imara.
Hivyo ameiomba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuweka
vituo vya polisi katika kila baadhi ya shehia kwa lengo la kukomesha vitendo vya udhalilishaji kwa
wanawake na watoto ambavyo hivi sasa
vinazidi kushamiri ndani ya mitaa na
kujenga khofu kwa jamii hasa ukatili wa
kupigwa mapanga na visu na kutaka sheria
kali itumike.
Nae Katibu wa UWT Wilaya ya Amani Sufiya Ubwa Mamboya amesema
tumuunge mkono Rais wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa
kuwataka viongozi wa majimbo washuke chini kwa wanachama ili kuweza kusikiliza
changamoto zao na kukaa pamoja katika
kuzitatua.
“Wamefanya kazi kubwa walipokuwa na nguvu zao hadi sasa
hawajiwezi tena wanahitaji kusaidiwa kwa kuwapitiwa huduma ambazo wanazihitaji.
Kwa upande wao wagonjwa hao wameishukuru kamati hiyo kwa
kuwatembelea na kuwafariji na wameomba iwe endelevu na kuwataka na viongozi wa juu kuwatembeleya.
Pia wamewaomba viongozi walioko hivi sasa katika jumuiya ya
UWT kufanya kazi kwa mashirikiano kama walivyofanya wao wakati wa uzima wao,
kwani wakifanya hivyo kutaweza kukuza chama na jumuiya kwa vizuri zaidi.
No comments:
Post a Comment