Habari za Punde

Ziara ya Waziri wa Elimu Zanzibar Mhe.Simai Mohammed Said Chuo Cha Mafunzo ya Amali Nchini Qatar.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Simai  Mohammed Said amefanya ziara katika Chuo cha Mafunzo ya Amali cha NORTH ATLANTIC cha Qatar na kufanya mazungumzo na Rais wa Chuo hicho, Dr Salem Al-Naemi.

Katika mazungumzo yao, wamekubaliana kujenga mashirikiano ya kielimu kwa ajili ya wanafunzi wa Zanzibar.

Mazungumzo hayo yataendelezwa kupitia Wizara ya Elimu pamoja na Ubalozi wa Tanzania.

Chuo hicho kinafundisha fani mbalimbali zikiwemo ufundi na uhandisi.






No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.