Habari za Punde

Mhe Hemed aupongeza uongozi wa Chuo Kikuu cha Bugema kwa kuwafariji waatihirika wa ajali ya Basi

Makamu wa Pili wa Rais Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akizungumza na uongozi wa BUGEMA UNIVERSITY uliofika Afisini kwake Vuga kujitambulisha na kubadilishana nae mawazo, Uongozi huo umekuja Zanzibar kwa ajili ya kuzifariji familia za Wahanga wa ajali ya Basi iliotokea Juni 02, mwaka huu Mkoani Shinyanga.
 

Na Kassim Abdi, OMPR

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abbdulla aliupongeza uongozi wa Bugema University  kutoka Uganda kwa  kuja kuwaona wanafunzi waliojeruhiwa kufuatia ajali ya basi iliotokea Mkoani Shinyanga Juni 02 Mwaka huu.

Mhe. Hemed alieleza hayo wakati alipofanya mazungumzo na uongozi wa chuo hicho uliofika ofisini kwake vuga kwa ajili ya kujitambulisha na kubadilishana mawazo kuhusina na masuala  mbali mbali ya kitaaluma

Alisema kuwa, serikali ya Mapinduzi Zanzibar  kupitia wizara ya afya inaendelea kuwahudumia  kwa karibu  wale wote waliopata ajali iliosababisha majeraha na wengine kupoteza  viungo ili kuimarisha Afya zao.

Alifafanua kuwa, Serikali  itaendelea kuwahudumia  wahanga hao kwa lengo la kuziimirisha Afya zao ili waendelee na majukumu yao katika kulitumikia taifa.

Aidha, Makamu wa Pili wa Rais aliuhakikishia uongozi wa BUGEMA UNIVERSITY kwamba serikali zote mbili  zitaendelea kushirikiana na chuo hicho katika kuhakikisha azma iliokusudiwa ya kuwataarisha wanafunzi kuwa wataalamu bora kupitia kada ya Afya iweze kufikiwa.

Nae Makamu Mkuu wa chuo hicho Prof.  PAUL KATAMBA alimueleza Makamu wa Pili wa Rais kuwa, uongozi wa chuo umeamua kuja  Zanzibar kwa lengo la kuziona na kuzifariji famila za wahanga pamoja na familia za wafiwa.

Pia Prof KATAMBA alisema kuwa kufuatia wahanga wa ajali waliopo Zanzibar kwa sasa chuo kimeamuwa kuja na utaratibu maalum wa masomo kwa kutumia njia ya mtandao (Online Study), njia ambayo itawawezesha wanafunzi hao kumalizia masomo yao wakiwa zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.