Habari za Punde

Serikali ina mkakati wa kuandaa mpango wa matumizi bora ya ardhi

Katibu Mkuu Afisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uweklezaji anaeshughulikia masuala ya Uchumi na Uwekezaji akizungumza na wataalamu wa kampuni ya CRM Consultant Ltd wsaliofika Wizarani kufanya mazungumzo nae katika kuandaa vyema mpango kabambe wa matumizi bora ya ardhi katika eneo la uwekezaji Fumba (Master Plan)


Na Saadam Seif -  Arkuu

Katibu Mkuu anaeshuhulikia masuala ya Uchumi na Uwekezaji  Afisi Ya Rais Kazi Uchumi Na Uwekezaji Habiba  Hassan Omar amesema serikali ina mpango wa kuandaa mpango wa matumizi bora ya ardhi kutika kuandaa miji yenye ubora na urahisi wa shughuli mbali mbali.

Ameyasema hao afisini kwake Mwanakwerekwe  Wilaya ya Magharib B wakati akizungumza na  wataalamu wa  kampuni ya Crm Land Consultant Ltd  kwa lengo la kujadiliana juu ya kuandaa mpango kabambe wa matumizi bora ya ardhi katika eneo la uwekezaji Fumba (Master Plan)

Katibu Habiba amesema ni mapendekezo ambayo Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeyapokea na imedhamiri kulifanyia kazi suala hilo na itahakikisha inabadilishina maoni na wadau mbali mbali wa masuala hayo ili kuona kwa namna gani mpango huo unafanikiwa katika utekelezaji wake.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa  kampuni ya Crm Land Consultant Ltd  Dk Clara kweka amesema lengo la kuzungumza pamoja na katibu huyo kutawasaidia kuandaa vyema mpango huo ambao utasaidia kwa kiasi kikubwa katika mpango wa serikali wa kuandaa mipango miji.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.