Naibu
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Pauline Gekul akiongea na
wanamichezo na mashabiki wa michezo wakati wa kufunga mashindano ya ligi ya
Chemchem Cup Desemba 24, 2021 katika kijiji cha Vilima Vitatu kata ya Nkaiti
iliyopo katika wilaya ya Babati Vijijni mkoani Manyara
Na Eleuteri Mangi, WUSM, Babati
Wakurugenzi
na Maafisa Michezo katika halmashauri zote nchini wametakiwa kutenga fedha kwa
ajili ya kukarabati viwanja vya michezo ili kuhakikisha michezo inachezwa
kuanzia ngazi ya chini hadi kitaifa.
Naibu
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Pauline Gekul ametoa rai hiyo Desemba
24, 2021 katika kijiji cha Vilima Vitatu kata ya Nkaiti iliyopo katika wilaya
ya Babati Vijijni mkoani Manyara wakati wa kufunga mashindano ya ligi ya Chemchem
Cup ambayo imeshirikisha vijiji 10 wanachama wa jumuiya ya uhifadhi wanyama
Kurunge.
Lengo
la mashindano hayo ni kuhamasisha jamii kuhifadhi wanyama pori na kutunza
mazingira katika maeneo yanayozunguka hifadhi za Tarangire na Ziwa Manyara.
“Sisi
kama Wizara tumeanza kutenga fedha kwa ajili ya Mfuko wa Maendeleo ya Michezo,
tumeanza kupunguza kodi kwenye vifaa vya michezo, tumeanza na nyasi za bandia
katika mwaka huu wa fedha na mmesikia Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan
ametupa maelekezo pia tukae na wenzetu wa Wizara ya Fedha tuone ni kwa kiasi
gani vifaa vya michezo vitapungua bei ili huku chini tuweze kumudu michezo”
amesema Mhe. Gekul.
Naibu
Waziri Gekul amewataka Wakurugenzi wa halmashauri waone sababu ya kukarabati
viwanja hivyo kwa kuwa vipo chini ya Madiwani, Mwenyekiti wa halmashauri na
chini ya kata na hivyo vikarabatiwe kwa kushirikiana kwa pamoja na wadau
wakiwemo wawekezaji ambao wapo maeneo mbalimbali nchi nzima.
Ili
kuhakikisha michezo inachezwa nchi nzima, Naibu Waziri amesema kuwa viwanja
vingi vipo chini ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI), jukumu hilo siyo lao peke yao bali ni la Serikali nzima ambapo
wanashirikiana kuhakikisha azma hiyo inafikiwa na inakuwa na tija kwa mtu mmoja
mmoja na taifa kwa ujumla.
“Mashindano
haya yawe ni chachu ya kupata timu ya mkoa ili kushiriki mashindano ya Taifa
Cup ambayo imeanza mwaka huu, naamini kupitia mashindano ya wilaya zote za mkoa
wetu tutapata wachezaji bora wanaounda timu ya mkoa wa Manyara, hatua hii
itayowafanya wachezaji wetu waongeze wigo mpana katika michezo na kuwafanya
waweze kusajiliwa kuweza katika vilabu vingine nje ya mkoa wetu” amesema Naibu
Waziri Gekul.
Naibu
Waziri Gekul amesisitiza kuwa Sera ya Michezo ya Taifa ya mwaka 1995 inaeleza
michezo kuwa siyo suala la mtu mmoja, michezo ni ya Serikali Kuu kupitia Wizara
yenye dhamana na michezo, ni ya Serikali za Mitaa, ni ya mtu mmoja mmoja na
michezo ni ya wanajamii nzima.
Ligi
hiyo ni ya saba na imegharimu zaidi ya Sh. milioni 25 yakihusisha gharama za
uendeshaji, zawadi yakiwemo makombe kwa mshindi wa kwanza hadi wa tatu, timu
yenye nidhamu, mfungaji bora, golikipa bora pamoja na kocha bora katika ligi
hiyo ambayo ilishirikisha vijiji 10 ambapo timu ya Marcklione imeibuka kidedea
na kuwa mshindi wa kwanza katika fainali hizo kwa kuifunga timu ya Minjingu Fc
kwa jumla ya magoli 4-0.
Kwa
upande wake Mwekezaji wa Chemchem ambayo inatoa huduma ya wanyamapori ya
Burunge inayojumuisha vijiji 10 katika eneo hilo Bw. Nicolaus Negre amesema
lengo la mashindano hayo ni kuwaleta watu pamoja ili kuwahamasisha juu ya
kuwatunza wanyama pori pamoja na mazingira yanayowazunguka.
Aidha,
Bw. Nicolaus ameongeza kuwa mashindano hayo yamekuwa na hamasa kwa vijana wa
eneo hilo kwa kuwa yanawasaidia kuendeleza na kuonesha vipaji vyao hatua
inayowasaidia kuweza kusajiliwa na vilabu vingine.
Naibu
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Pauline Gekul (wa kwanza) akikagua
timu kabla ya kuanza kwa mechi ya fainali za mashindano ya ligi ya Chemchem Cup
iliyozikutanisha timu za Marcklione na Minjingu Fc ambapo timu Marcklione
imeifunga timu ya Minjingu Fc kwa magoli 4-0 Desemba 24, 2021 katika kijiji cha
Vilima Vitatu kata ya Nkaiti iliyopo katika wilaya ya Babati Vijijni mkoani
Manyara.
Mchezo wa fainali za mashindano ya ligi ya Chemchem Cup ambayo imezikutanisha timu za
Marcklione (waliovaa jezi ya bluu) na Minjingu Fc ambapo timu Marcklione
imeifunga timu ya Minjingu Fc kwa magoli 4-0 Desemba 24, 2021 katika kijiji cha
Vilima Vitatu kata ya Nkaiti iliyopo katika wilaya ya Babati Vijijni mkoani
Manyara.
Mwekezaji
wa Chemchem lodge ambaye pia ni mdhamini wa mashindano ya ligi ya
Chemchem Cup 2021 Bw. Nicolaus Negre akiongea na wananchi Desemba 24, 2021
katika kijiji cha Vilima Vitatu kata ya Nkaiti iliyopo katika wilaya ya Babati
Vijijni mkoani Manyara wakati wa kufunga mashindano hayo ambayo lengo lake ni
kuwahamasisha juu ya kuwatunza wanyama pori pamoja na mazingira
yanayowazunguka.
Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Pauline Gekul akimkabidhi Nahodha wa timu ya Marcklione katika kijiji cha katika kijiji cha Vilima Vitatu kata ya Nkaiti iliyopo katika wilaya ya Babati Vijijni mkoani Manyara Desemba 24, 2021 ambayo imeifunga timu ya Minjingu Fc kwa jumla ya magoli 4-0 katika mashindano ya ligi ya Chemchem Cup iliyoshirikisha vijiji 10 wanachama wa jumuiya ya uhifadhi wanyama yenye lengo la kuhamasisha jamii kuhifadhi wanyama pori na kutunza mazingira katika maeneo yanayozunguka hifadhi za Tarangire na Ziwa Manyara.
No comments:
Post a Comment