Habari za Punde

Naibu Waziri Ummy akabidhi vyerehani kwa kikundi cha wenye ulemavu Chamanangwe kisiwani Pemba

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Wenye Ulemavu) Mhe. Ummy Nderiananga pamoja na Mbunge wa Jimbo la Kojani na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Hamad Chande wakikabidhi chereani kwa mwakilishi wa kikundi cha watu wenye ulemavu Bi. Asha Issa Kombo (wa kwanza kushoto) wanaojifunza ushonaji wa nguo katika eneo la Chamanangwe Wilaya ya Wete Pemba. Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Baraza la Taifa la Watu Wenye Ulemavu Zanzibar Bw. Ussi Debe na wa pili kutoka kushoto ni Afisa Mdhamini Ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais Mhe. Amhed Aboubakar Mohamed.
Naibu waziri Ofisi ya Waziri Mkuu(Wenye Ulemavu) Mhe. Ummy Nderiananga akizungumza na wanakikundi wa Chamanangwe (wenye ulemavu) wanaojifunza ushonaji wa nguo, alipowatembelea na kukabidhi chereani sita katika eneo la hilo katika Wilaya ya Wete visiwani Pemba Januari 4, 2022.
Mbunge wa Jimbo la Kojani na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Hamad Chande akizungumza wakati hafla ya kukabidhi chereani sita katika eneo la Chamanangwe katika Wilaya ya Wete visiwani Pemba Januari 4, 2022.

Naibu waziri Ofisi ya Waziri Mkuu(Wenye Ulemavu) Mhe. Ummy Nderiananga pamoja na ugeni alioongozana nao wakiwa katika picha ya pamoja na wanakikuchi hao, mara baada ya zoezi la kukabidhi chereani hizo zinazolenga kuwawezesha katika shughuli za kujikwamua kiuchumi Chamanangwe katika Wilaya ya Wete visiwani Pemba

(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.