Habari za Punde

Viongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii Waaza Kazi Baada ya Kuapishwa.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Dkt. Maurus Msuha mara baada ya kuripoti ofisini  Mtumba jijini Dodoma baada ya kuteuliwa kwa mara nyingine katika nafasi hiyo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan. Anayeshuhudia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) (wa pili kulia).
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Francis Michael (wa pili kutoka kushoto) na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Juma Mkomi (wa nne kutoka kushoto) wakiwasili katika Ofisi za Wizara zilizopo Mtumba jijini Dodoma mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Francis Michael akifurahia jambo na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Leonard Mchau alipowasili kwa mara ya kwanza Ofisi za Wizara zilizopo Mtumba jijini Dodoma mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) wakimkaribisha Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Juma Mkomi katika Ofisi za Wizara zilizopo Mtumba jijini Dodoma mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.