Habari za Punde

Ufunguzi wa Jengo Jipya la Saccos ya Madareva wa Texi Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar.

Muonekano wa Jengo Jipya la Ushirika wa Madereva wa Taxi Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar lilopo Kiembesamaki Zanzibar.
Mkurugenzi Utumishi na Uwendeshaji Dk. Shaaban Hassan Haji akihotubia katika mkutano wa 11 wa ushirika wa madereva wa Taxi Uwanja wa Ndege uliofanuika katika Ukumbi wa Ushirikia huo Kiembesamaki ambapo Dk. Shaaban alimuwakilisha Mhe. Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi.
Wanachama wa ushirika wa madereva wa Taxi Uwanja wa ndege wakimskiliza Mkurugenzi Utumishi na uwendeshaji Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Dk. Shaaban Hssan Haji wakati akiufungua mkutano wa 11 wa ushirika huo uliofanyika katika  Ukumbi wa Ushirikia huo Kiembesamaki ambapo Dk. Shaaban alimuwakilisha Mhe. Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi.

Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Mhe. Rahma Kassim Ali amesema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inatambua na kuthamini mchango unaotolewa na ushirika wa madereva wa Taxi uwanja wa ndege katika kukuza hadhi na haiba ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Zanzibar.

Mkurugenzi utumishi na Uwendeshaji Dk. Shaaban Hassan Haji alieleza hayo kupitia hotuba  alioisoma kwa niaba ya Waziri wa ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi katika hafla ya mkutano wa 11 wa ushirika wa madereva wa Taxi uanja wa ndege uliofanyika katika ukumbi wa mkutano wa Ushirikahuo huo uliopo kiembe samaki  Jijini Zanzibar.

Aidha Mhe. Waziri aliwashauri wanaushirika wa umoja huo wa madereva kuendeleza na kuimarisha huduma zao kwa kuwa na mashirikiano ya  karibu na mamlaka ya viwanja vya ndege ili kuendelee kuwahudumia na kuwahakikisha usalama wa wageni.

 Kuhusiana na kupewa fursa za kutoa huduma katika viwanja vyote  Mhe. Waziri ailwataka madereva hao kuwa wavumilivu na aliwahakikishia  mkakati wa kuhamia jengo jipya la uanja wa ndege utakapokamilika serikali itazingatia na kutoa kipaombele kwa ushirika huo baada ya wizara kujiridhisha kwamba ushirika huo una uwezo na vigezo vya kutoa huduma bora.

“Niseme tu ni lazima ushirika ujipange zaidi ili dhamana mtakayopewa muweze kuitekeleza kwa ufanisi  na viwango vinavyotakiwa”Alisema Mhe. Waziri.

Pamoja na mambo mengine, Mhe. Waziri aliwahakikishia wanaushirika hao suala la malipo ya fidia litafanyika baada ya Wizara kufanya uhakiki wa deni hilo na kijiridhisha.

Akisoma risala kwa niaba ya wanaushirika Ndg. Maryam Said Soud alimuomba Mhe. Waziri kupitia wizara anayoisimamia kuendelea kuwapa fursa na kuwaamini kwa kuwapa nafasi ya kutoa huduma katika viwanj vyote kwani uwezo walionao ni wa kuridhisha.

Sambamba na hayo, Ndg. Maryam alimuomba  Mhe. Waziri kutoa msukumo wa kulipwa fedha wanazodai ambazo zilitumika kwa ajili ya ujenzi wa vyoo katika eneo la uegeshaji wa magari.

Akigusia changamoto zinazowakabili alisema ni uwelewa mdogo pamoja na ufinyu wa elimu ya ujasiliamali jambo linalosababisha kutofikiwa kwa malengo ya ushirika huo katika kuwaingizia kipato wanachama wake.

Ushirika wa madereva wa Taxi Uwanja wa ndege umeanzishwa februari 2003 na  una jumla ya wanachama mia moja na hamsini na tano (155) wakiwemo wanawake Arobaini (40) na wanaume mia  moja na kumi na tano (115).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.