Habari za Punde

Zoezi la usafi fukwe za Vumawimbi

MKUU wa Wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahaya, akizoa taka na kutia katika bero wakati wa zoezi la usafishaji wa Fukwe ya Vumawimbi, iliyopo kijiji cha Makangale Wilaya ya Micheweni ikiwa utangazaji wa Ufukwe huo kwa watalii.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

WATENDAJI wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Chake Chake Rashid Abdalla Rashid na Mkurugenzi wa Baraza la Mji Wete Salma Abouu Hamad, wakifagia ufukwe wa Vumawimbi ikiwa ni ishara ya zoezi la ufanyaji usafi katika fukwe hiyo.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MKUU wa Mkoa wa Kusini Pemba na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Mattar Zahor Masoud (kushoto) akifukiwa takataka katika moja ya shimo walilolichimba, wakati wa zoezi la ufanyaji usafi ufukwe wa Vumawimbi, katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Chake Chake Abdalla Rashid Ali na Mkuu wa Wilaya ya Wete Mgeni Khatib Yahara.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MKUU wa Wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya akimimina taka katika bero kwa ajili ya kwenda kutupwa sehemu maalumu, wakati wa zoezi la ufanyaji usafi katika Fukwe ya Vumawimbi Wilaya ya Micheweni.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MKUU wa Mkoa wa Kusini Pemba na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Matar Zahor Masoud, (katikati) akiwaongoza viongozi mbali mbali wa serikali katika kusafisha ufukwe wa Vumawimbi Wilaya ya Micheweni, ikiwa ni Zoezi la Kufanya usafi katika fukwe hiyo iliyoko Micheweni.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.