Habari za Punde

Ziara ya Waziri wa Uchumi wa Buluu Kisiwa cha Mnemba.

Na Kijakazi Abdalla. Maelezo Zanzibar. 24/03/2022

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema itachukua hatua za makusudi ili kukinusuru kisiwa cha Mnemba  kisiendelee  kuchukuliwa na bahari  li kiendelee kuleta haiba  kwa  watalii.

Haya ameyasema Waziri wa Uchumi wa Bluu na Uvuvi Suleiman Masoud Makame  wakati  alipofanya  ziara katika  kisiwa  hicho na kuona  jinsi  mabadiliko  ya  tabia  ya nchi yalivyokiathiri  kisiwa hicho.

Ameema  ikiwa serikali haitachukua  jitihada hizo basi kisiwa hicho kitaendelea  kupotea   na kupoteza  haiba ya nchi hasa historia ambayo imedumu kwa muda mrefu.

Aidha amesema  kisiwa hicho kina historia ndefu ya utalii na eneo moja lenye manufaa  katika  kukuza  pato la serikali na eneo la hifadhi ya mazingira ya baharini.

Vilevile amesema  tayari eneo hilo limeshaathiriwa kwa kiasi kikubwa na maji na tayari bahari imeshachukua  mita 30 hadi 40 ya kisiwa hicho.

Hata hivyo alisema  atashirikiana  na  serikali ikiwemo Mamlaka ya Mazingira, Uchumi wa Bluu na Uvuvi na Idara ya Misitu kuona wanakinusuru kisiwa hicho.

Naye, Meneja wa mradi wa kisiwa cha Mnemba, Jonathan Braack, alisema  eneo la upande wa kulia  la bahari  ambalo lilikuwa  ni nchi kavu hivi sasa limeshavamiwa  na maji ya bahari.

Alisema, takriban mita 50 ambazo zilikuwa  bangaloo wanazoishi watu tayari zimeshavamiwa  na  maji ya  bahari  hivyo ni vyema kwa serikali  kuchukua  jitihada  za kukinusuru kisiwa hicho kisiendelee kuathiriwa  na  maji ya bahari.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.