Habari za Punde

Waziri Mhe.Riziki Pembe Juma Alaani Kitendo cha Udhalilisha cha Mtoto Aliyedhalilishwa na Baba Yake Mzazi.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Zanzibar Mhe Riziki Pembe Juma, akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vilioko Zanzibar kuhusiana na kutoa taarifa za kukamatwa kwa mtuhumia wa kitendo cha udhalilshaji wa mtoto wake wa kumzaa mtuhumiwa Ndg.Kheri Mkombe Abdalla,ili kufikishwa katika vyombo vya sheria. 
Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vilioko Zanzibar wakifuatilia taarifa ikitolewa na Wairi wa Jamii,Jinsia Wazee na Watoto Zanzibar Mhe.Riziki Pembe Juma.(hayupo pichani) kuhusia na kusakwa kwa mtuhumiwa na kitende cha kumdhalilisha mtoto wake.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Riziki Pembe Juma ameiomba jamii kushirikiana katika kutoa taarifa za kupatikana kwa mtuhumiwa Kheri Mkombe Abdallah anaetuhumiwa kumfanyia kitendo cha udhalilishaji  mtoto wake ili kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Akizungumza na vyombo vya habari kuhusiana na tukio hilo lililotokea hivi karibuni amesema kutokutowa taarifa hizo kwa anaezifahamu kunaashiria kuunga mkono kitendo alichokifanya ambacho kinapaswa kulaaniwa na jamii nzima.

Amesema kukithiri kwa vitendo hivyo ndani ya jamii kumepelekea kuathiri maadili ya jamii nzima hivyo wananchi wanapaswa kushirikiana na Serikali katika kuona inalaani vitendo hivyo kwa kuvifichua ili kuvikomesha na  kutoendelea kuwepo.

Akizungumzia kuhusiana na kutokukidhi haja kwa sheria zilizopo sasa juu ya makosa hayo Mhe Riziki amefahamisha kuwa Wizara kwa kushirikiana na wadau wa masuala ya sheria imeanza kufanya mapitio ya sheria za sasa ili kutambua mapungufu yaliyopo na hatimae kupatikana sheria zitakazokidhi mahitaji.

Aidha ameshauri jeshi la polisi nchini kutumia saikolojia zaidi wakati wanapowahoji watoto waliofanyiwa vitendo hivyo ili kuepusha kuwatia hofu na kupelekea kutoa taarifa zenye mapungufu zinazoweza kuathiri mwenendo wa kesi katika hatua za awali.

Wakati huo huo Mhe Riziki amesema Wizara inalaani vikali juu ya tukio hilo na haitalifumbia macho, ambaoo ameahidi kuchukuliwa  hatua za kisheria wakati mtuhumiwa wa tukio hilo atakapokamatwa.

Nao Maafisa Ustawi wa Wilaya mbali mbali za Unguja, wamesema pamoja na kutoa elimu ya kuihamasisha jamii kutokuficha makosa hayo yanapotokea lakini bado kumekuwa na vikwazo katika kufuatilia kesi hizo ikiwemo kukosa ushirikiano hasa kwa makosa ya udhalilishaji yanayofanyika ndani ya familia.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.