Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ameushukuru Mfuko wa Misaada wa Sheikh Zayed bin Sultan Al
Nahyan kwa kuiunga mkono Zanzibar katika kuimarisha sekta ya afya, elimu pamoja
na ustawi wa Jamii.
Rais
Dk. Mwinyi alitoa shukurani hizo leo Ikulu Zanzibar mara baada ya kushuhudia
utiaji saini kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na Mfuko wa Misaada
ya Sheikh Zayed bin Sultan Al Nahyan kutoka nchi za Jumuiya ya Falme za Kiarabu
(UAE), ambapo mfuko huo utasaidia katika sekta ya elimu, afya na ustawi wa
Jamii.
Akitoa
shukurani hizo, Rais Dk. Mwinyi alisema kwamba Mfuko huo umechukua uwamuzi
stahikli wa kuisaidia Zanzibar katika maendeleo yake ikiwa ni pamoja na azma ya
kujenga skuli mbili, kituo cha wazee cha kisasa pamoja na Hospitali.
Aliongeza
kuwa hatua hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa kuunga mkono juhudi za Serikali
katika kuendeleza ujenzi wa miradi ya maendeleo unaotekelezwa hivi sasa.
Rais
Dk. Mwinyi alitumia fursa hiyo kutoa shukurani kwa Rais wa nchi za Jumuiya ya
Kiarabu (UAE) Sheikh Mohamed bin Zayed Al Nahyan kwa kuendelea kuiunga mkono
Zanzibar katika kuimarisha miradi mbali mbali ya maendeleo.
Nae
Waziri wa Fedha na Mipango Saada Mkuya Salum alieleza kuwa Mfuko huo wa Misaada
wa Sheikh Zayed bin Sultan Al Nahyan una azma ya kujenga skuli mbili ikiwemo ya
Muembeladu na Mtopepo, kituo cha kisasa cha wazee kitakachokuwa na nyumba za
watendaji wake pamoja na kujenga hospitali. kisasa.
Waziri
Mkuya alisema kuwa nchi za Jumuiya ya Kiarabu (UAE), zimekuwa na mahusiano
mazuri na Zanzibar hivyo hatua hiyo itasaidia utekelezaji wa mikakati katika maeneo
aliyoyapa kipaumbe Rais Dk. Mwinyi.
Hivyo,
aliahidi kwamba Wizara yake itahakikisha inatoa ushirikiano mkubwa kwa Taasisi
hiyo ili iweze kufikia malengo iliyojiwekea.
Mapema
Mkuu wa Taasisi hiyo ya Misaada ya Sheikh Zayed bin Sultan Al Nahyan, Sheikh Hamad Salem bin Kardous Al Amer
aalisema kwamba Jumuiya ya nchi za Falme za Kiarabu (UAE) ina uhusiano Mwema na
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwenmo Zanzibar.
Alisema
kuwa misaada hiyo ni hatua za kiongozi mkuu wa nchi hiyo katika kuiunga mkono
Zanzibar kwani anatambua uhusiano na ushirikiano uliokuwepo ambao kuna haja ya
kuendelezwa na kudumishwa.
Aidha,
kiongozi huyo alitumia fursa hiyo kumpongeza Rais Dk. Mwinyi kwa hatua zake za
kuendeleza mahusiano na mashirikiano mema yalipo kati ya Zanzibar na (UAE)
sambamba na ukarimu mkubwa alionao kwa nchi za Umoja huo.
Aliongeza
kuwa hatua hiyo pia itasaidia kuanzisha ziara kati ya pande mbili hizo
zitakazosaidia kuimarisha uhusiano na ushirikiano mkubwa uliopo huku akimuomba
Mwenyezi Mungu kuipa Zanzibar maendeleo makubwa yenye amani ndani yake.
Zoezi
hilo la utiaji saini lililoshuhudiwa na Rais Dk. Mwinyi lilifanyika kati ya
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mfuko wa Misaada wa Sheikh Zayed bin
Sultan Al Nahyan ambapo kwa upande wa Serikali alietia saini ni Katibu Mkuu
Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Dk. Juma Malik Akil na kwa upande wa Mfuko huoa
alietia saini ni Sheikh Hamad Salem bin Kardous Al Amer.
Viongozi
mbali mbali walihudhuria akiwemo Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali
Maulid, Balozi wa (UAE) nchini Tanzania Khaalifa Abdulrahman Mohamed Al
Marzooqi, Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama,
Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi, Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh
Othman Ngwali, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Injinia
Zena Ahmed Said, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Mwinyi Talib Haji, Mkuu wa Mkoa
wa Mjini Magharibi Idrissa Kitwana Mustafa pamoja na viongozi wengine wa
Serikali.
Imetayarishwa na
Idara ya Mawasilaino,
Ikulu Zanzibar.
No comments:
Post a Comment