Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi Ameongoza Maelfu ya Wananchi Katika Maziko ya Kaka Yake Marehemu Hassan Ali Hassan Mwinyi Katika Kijiji cha Mangapowani leo 31-8-2022.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Wananchi na Ndugu katika kisomo cha hitma na dua kumuombea Kaka yake Marehemu Hassan Ali Hassan Mwinyi iliyofanyika kijijini kwao Mangapwani Wilaya ya Kaskazini “B” Unguja  na (kushoto kwa Rais) Mtoto wa Marehemu Ibrahim Hassan Ali Hassan, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Alhaj Othman Masoud Othman na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhaj Hemed Suleiman Abdulla, wakijumuika katika kisomo hicho leo 31-8-2022.




RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Wananchi na Viongozi mbalimbali wa Serikali na Vyama vya Siasa katika Sala ya Jeneza ya Marehemu Hassan Ali Hassan Mwinyi Kaka yake iliyofanyika Kijijini kwao Mangapwani Wilaya ya Kaskazini “B” Unguja leo 31-8-2022, na (kulia kwa Rais) Rais Mstaafu wa Tanzania Alhaj Ali Hassan Mwinyi,Mbunge wa Jimbo la Mahonda Mhe. Abdalla Hassan Mwinyi  na Spika wa Baraza la Wawakilishi Alhaj Zuberi Ali Maulid 
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na kupewa mkono wa pole na Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo Mhe. Zito Zuberi Kabwe, wakati wa maziko ya Kaka yake Marehemu Hassan Ali Hassan Mwinyi yaliyofanyika Kijiji kwao Mangapwani Wilaya ya Kaskazini “B” Unguja leo 31-8-2022

RAIS Mstafu wa Tanzania Alhaj Ali Hassan Mwinyi akiweka mchanga katika kaburi la  Mtoto wake Marehemu Hassan Ali Hassan Mwinyi maziko yaliofanyika leo 31-8-2022 Mangapwani Wilaya ya Kaskazini “B” Unguja leo 31-8-2022
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiweka mchanga katika kaburi la Marehemu Kaka yake Hassan Ali Hassan Mwinyi, wakati wa maziko hayo yaliyofanyika leo 31-8-2022 katika Kijiji cha Mangapwani Wilaya ya Kaskazini “B”Unguja




RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akishiriki katika kuitikia  dua ya kumuombea Marehemu Hassan Ali Hassan Mwinyi ikisomwa na Sheikh Shariff (hayupo pichani) baada ya kumalizika kwa maziko hayo yaliyofanyika katika Kijiji cha Mangapwani Wilaya ya Kaskazini “B” Unguja leo 31-8-2022 na (kushoto kwa Rais) Rais Mstaafu wa Tanzania Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhaj Hemed Abdulla Suleiman na Rais Mstaafu wa Zanzibar Alhaj Dkt.Amani Karume


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na kuagana na Rais Mstaaf wa Zanzibar Alhaj Dkt.Amani Karume, baada ya kumalizika kwa maziko ya Kaka yake Marehemu Hassan Ali Hassan Mwinyi yaliyofanyika katika Kijiji cha Mangapwani Wilaya ya Kaskazini “B” Unguja leo 31-8-2022, na (kushoto kwa Rais) Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhaj Hemed Abdulla Suleiman


















 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.