Habari za Punde

Watanzania na Waafrika kwa ujumla kuunga mkono jitihada za Serikali zao za kuhamasisha kununua huduma na bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya ndani ya Afrika.

MAKAMU wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman akizungumza wakati akifunga mkutano wa Kimataifa wa Wanawake na vijana  katika bishara chini ya Mkataba wa Itifaki ya Eneo huru la Biaahara Afrika huko katika Kituo cha  Mikutano cha Kimataifa Cha Mwalimu Julius Nyerere Mjini Dar es e Salaam Leo tarehe 14.09.2022.  Picha Na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Kitengo cha Habari 
MAKAMU wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman akizungumza wakati akifunga mkutano wa Kimataifa wa Wanawake na vijana  katika bishara chini ya Mkataba wa Itifaki ya Eneo huru la Biaahara Afrika huko katika Kituo cha  Mikutano cha Kimataifa Cha Mwalimu Julius Nyerere Mjini Dar es e Salaam Leo tarehe 14.09.2022.  Picha Na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Kitengo cha Habari 
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman akizungumza  akibadilishana mawazo na Katibu Mtendaji  wa Sekretariet ya Eneo huru la Biashara Afrika Kabla ya Mhe. Othman kuufunga rasmi mkutano wa Kimataifa wa Wanawake na vijana  katika bishara chini ya Mkataba wa Itifaki ya Eneo huru la Biaahara Afrika huko katika Kituo cha  Mikutano cha Kimataifa Cha Mwalimu Julius Nyerere Mjini Dar es e Salaam Leo tarehe 14.09.2022.  Picha Na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Kitengo cha Habari .
 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk Hussein Mwinyi amewataka Watanzania na Waafrika kwa ujumla kuunga mkono jitihada za Serikali zao za kuhamasisha kununua huduma na bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya ndani ya Afrika.

Mhe. Rais Mwinyi ameyasema hayo jijini Dar es Salaam katika Hotuba iliyosomwa kwa Niaba yake na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, alipofunga Mkutano wa kimataifa wa Wanawake na Vijana katika Bishara chini ya Mkataba  wa Eneo Huru la Biashara Afrika.

Mhe. Mwinyi amesema kwamba hatua hiyo ya kupenda bidhaa za ndani itasaidia kutimiza malengo ya Biashara chini ya Mkataba wa Eneo huru la Biashara Afrika ya kukuza bishara na Viwanda Barani Afrika katika jitihadaza kukuza na kuenua uchumi na maendeleo kwa jumla.

Amesema kewamba Kaulimbiu ya mkutano huo ya "Wanawake na Vijana ni  Injini ya Biashara chini ya Mkataba wa Eneo Huru la Biashara la Afrika, iwapo itatekelezwa kwa vitendo itachangia   sana wanawake wengi zaidi kushiriki katika shughuli za biashara  na kupelekea uchumi kuimarika na kukua zaidi.

Amefahamisha kwamba kuwepo ushiriki mkubwa wa wanawake kwenye mkutano huo ambao umafanyika sambamba na maonesho ya kibiashara ni  unaonesha umuhimu kwa nchi za afrika katika kuona ushiriki bora wa wanawake kwenye harakati za biashara kwa lengo la kukuza uchumi na maendeleo yao.

Amesema kwamba mkutano huo umeonesha kuwepo mwamko mkubwa   wa ushiriki wa makundi ya wanawake na vijana katika jitihada za ukuaji wa uchumi Barani Afrika hasa kupitia Sekta ya Biashara.

Aidha amesema kwamba Mkutano na Maonesho ya Biashara yaliyofanyika yametoa elimu kubwa na kutengeneza fursa pana kwa washiriki hao kubadilishana uzoefu na taarifa muhimu za kibiashara na kuwataka kuendelea kubadilisha uzoefu ili kuzitumia vyema fursa za kibiashara zilizopo katika soko huru la Afrika.

Amesema mkutano huo pia umetoa fursa ya kuwepo mjadala maalum na kutoa mapendekezo  kuhusu itifaki ya Wanawake na Vijana katika Biashara chini ya Mkataba wa Eneo Huru la Biashara la Afrika.

Amefahamisha kuwa maoni na mapendekezo yaliyotolewa yatazingatiwa katika uandaaji wa Itifaki hiyo ili iweze kusaidia kuongeza ushiriki na mchango mkubwa zaidi wa Wanawake na Vijana kwenye biashara kwa kutumia ipasavyo fursa zitokanazo na Mkataba wa Eneo Huru la Biashara la Afrika.

Naye Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia wazee na Watoto Zanzibar Mhe. Riziki Pembe Juma, amesema kwamba sera za kiuchumi na biashara zinazotungwa na serikali za Afrika hivi sasa zinajielekez zaidi kuunga mkono jitihada za ushiriki mpana wa wanawake na vijana katika kukuza uchumi kupitia shughuli za kibishara.

Kwa Upande wake waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar Omar Said Shaaban, amesema kwamba changamoto kubwa iliyopo katika sekta ya biashara kwa vijana wa Afrika  sio sera na sharia bali ni namna ya kuzitafsiri katika kuchangia kuimarisha biashara na kuendeleza ukuaji wa uchumi na maendeleo.

Naye Katibu Mtendaji wa Sekretariet wa Eneo Huru la Biashara Afrika Bwana Mamkele Mene, amesema kwamba mkutano huo uliofanyika kwa ufanisi ni muhimu kwa kuwa mjadala wake utasaidia sana katika kupatikana suluhisho la changamotio mbali mbali za kibiashara zinazojitokeza katika nchi za Afrika.

Imetolewa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo cha Habari leo tarehe 14.09.22.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.