Mhariri Mtendaji Shirika la Magazeti ya Serikali Ali Mwadini akiwasilisha mada kuhusu Mafanikio ya Serikali kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo Maafisa Habari na Mawasiliano wa Wizara mbalimbali za Serikali huko Ukumbi wa Studio Rahaleo Zanzibar
Mhariri Mtendaji wa Shirika la Magazeti ya Serikali Ali Mwadini akionyesha mfano wa kijarida maalum cha Serikali “Neema Zetu” kitakachotolewa na Shirika la Magazeti chini ya Wizara ya Habari kinachoelezea utendaji wa Serikali , wakati akiwasilisha mada ya mafanikio ya Serikali kupitia vyombo vya Habari na mitandao ya kijamii katika mafunzo ya kuwajengea uwezo Maafisa Habari na Mawasiliano wa Wizara mbalimbali za Serikali huko Ukumbi wa Studio Rahaleo Zanzibar.
Maafisa Habari na Mawasiliano wa Wizara mbalimbali za Serikali wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo , yaliyoandaliwa na Idara ya Habari Maelezo Zanzibar katika Ukumbi wa Studio Rahaleo.
Afisa Mawasiliano Wizara ya Nchi (OR) Fedha na Mipango Asha Saleh akichangia mada wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo Maafisa Habari na Mawasiliano wa Wizara mbalimbali za Serikali huko Ukumbi wa Studio Rahaleo Zanzibar, mafunzo hayo yameandaliwa na Idara ya Habari Maelezo Zanzibar.
Afisa Mawasiliano Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Kassim Abdi akichangia mada wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo Maafisa Habari na Mawasiliano wa Wizara mbalimbali za Serikali yaliyofanyika katika Ukumbi wa Studio Rahaleo, mafunzo hayo yameandaliwa na Idara ya Habari Maelezo Zanzibar.
Afisa Mawasiliano Ikulu Mwatima Rashid Issa akichangia mada wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo Maafisa Habari na Mawasiliano wa Wizara mbalimbali za Serikali yaliyoandaliwa na Idara ya Habari Maelezo Zanzibar huko Ukumbi wa Studio Rahaleo Zanzibar.
Afisa Utumishi Wizara ya Nchi, (OR) Katiba,Sheria, Utumishi na Utawala Bora Bakari Khamis Muhidini akiwasilisha mada kuhusu Muundo wa Utumishi wa Kada ya Maafisa Habari na Mawasiliano wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo Maafisa Habari na Mawasiliano wa Wizara mbalimbali za Serikali huko Ukumbi wa studio Rahaleo Zanzibar.
No comments:
Post a Comment