Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis
Hamza Khamis amesema Serikali imechukua hatua mbalimbali ikiwemo kutekeleza
miradi ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
Amesema hayo wakati akizungumza kwa nyakati tofauti mkoani Songwe wakati
wa ziara ya Kamati ya Mawaziri nane wa Wizara za
Kisekta inayoshughulikia migogoro ya matumizi ya ardhi katika vijiji.
Akizungumza na uongozi wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Khamis alisema Serikali
kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais inatekeleza miradi hiyo ikiwemo uchimbaji
visima katika maeneo yenye ukame ili wananchi waweze kupata maji kwa ajili ya
matumizi.
Alisema pia Serikali inatekeleza miradi ya kuwezesha upatikanaji wa
majiko banifu ambayo yanasaidia kupunguza au kuondosha kabisa vitendo vya
ukataji miti kwa ajili ya kuni na mkaa sambamba na kuhamasisha matumizi ya mkaa
mbadala.
Katika kuhakikisha kuwa nchi yetu inaondokana na ukame ambao na zoezi la
upandaji miti linaendelea kutekelezwa kwa kupanda miti milioni moja na nusu kwa
kila halmashauri.
“Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais imeanzisha na inasimamia Kampeni
Kabambe ya Hifadhi na Usafi wa Mazingira, Kampeni ya Soma na Mti ambayo
inahusisha wanafunzi wa shule na vyuo kupanda miti kwa lengo la kukabiliana na
athari za mabadiliko ya tabanchi,” alisema Mhe. Khamis.
Akizungumza na wananchi wa kitongoji cha
Ikanka kijiji cha Itumba wilayani ileje alisisitiza wananchi kuendelea
kupanda miti katika maeneo waliyoachiwa ili kutunza mazingira.
Naibu Waziri Chilo alisema kuwa miti mingi inaonekana imekatwa hali
inayosababisha ukosefu wa mvua katika maeneo mbalimbali hapa nchini.
Tayari kamati ya mawaziri nane wa wizara za kisekta imeshatembelea mikoa
kumi na tisa kati 26 kamati imeshapeleka mrejesho wa maamuzi ya baraza la
mawaziri na inaendelea na ziara yake kwenye mikoa ya Mbeya, Iringa, Njombe na Ruvuma.
No comments:
Post a Comment