Habari za Punde

Mkutano Mkuu wa Tano wa Madrasatul Hayaatul Atfaal

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman akisalimiana na baadhi ya Viongozi wa Madrasat Hayaatul Atfaal ya Baghani Wete Pemba wakati alipowasil katika ukumbi wa Banquate  Kiembe Samaki  wilaya ya Magharib B Unguja kwa ajili ya ufunguzi wa Mkutano wa Tano wa mwaka wa Madrasat  Hayaatul Atfaal ya Baghani Wete Pemba iliofanyika 25.12.2022.

Baadhi ya wanafunzi Waliohudhuria katika Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Madrasat Liaatfal ya Baghani Wete Pemba wakiwa katika Picha ya Pamoja wakisoma dua ya Kumkaribisha Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman  alipowasili ili kuufungua rasmi mkutano huo huko katika ukumbi wa Banquate  Kiembe Samaki  wilaya ya Magharib B Unguja leo tarehe 25.12.2022. Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Kitengo cha habari.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman akipokea zawadi kutoka mmoja wa Viongozi wa Madrasat Hayaatul Atfaal ya Baghani wete Pemba  wakati Mhe. Othman alipowasil katika ukumbi wa Banquate  Kiembe Samaki  wilaya ya Magharib B Unguja ili kufungua Mkutano wa Tano wa mwaka wa Madrasa hiyo leo tarehe 25.12.2022. Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Kitengo cha habari.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Alhaj Othman Masoud Othman akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Washiriki na Viongozi mbali mbali waliohudhuria Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Madrasat Liaatfal ya Baghani Wete Pemba baada ya kumalizika kwa ufunguzi wa mkutano huo uliofanyika  katika ukumbi wa Banquate  Kiembe Samaki  wilaya ya Magharib B Unguja

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman akifungua Mkutano wa Tano wa mwaka wa Madrasat  Hayaatul Atfaal ya Baghani Wete Pemba  uliofanyika Katika ukumbi wa Banquate Kiembe Samaki wilaya ya Magharib B Unguja 25.12.2022.

Na.OMKR.

MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amesema Zanzibar imekabiliwa na janga kubwa la kimaadili na kusababisha kuwepo baadhi ya watumishi wasomi wanaofanya vitendo vya kuiibia  nchi mamilioni ya fedha kupitia dhamana zao za kazi.

Mhe. Othman ameyasema hayo huko Kiembesamaki Wilaya ya Magharib Unguja katika ukumbi wa Banquate  alipofungua Mkutano Mkuu wa tano wa mwaka wa  Madrsat  hayaatul atfaal  ya Baghani Wete Pemba.

Mhe. Othman amsema watu wanaofanya vitendo vya kuiba mali za serikali sio wale walioishia darasa dogo la elimu lakini wengi wao ni wasomi wenye mashahada ya juu na wanafanya hivyo kutokana na kutokana wazee kutokuwa na maadili mema yanayotokana na muongozo wa dini.

Ameitaka jamii kuhakikisha kwamba wanawaandaa vijana katika maadili kwa kuwafundisha tabia njema za kumcha mwenyezimungu muumba ili waweze kuwa watu wema ndani ya nchi yao.

Amefahamisha kwamba jukumu la malezi bora yenye maadili ni wajibu  wa wazazi wenyewe na Kwamba sio busara jambo hilo kuachwa kwa walimu pekee ama kuonekana kwamba ni jukumu la serikali zaidi badala ya wazazi na jamii kwa jumla.

Ameitaka jamii kuwekeza katika kukifanya kizazi kisiihame kuraani na maamuru yake  kwa kufanya hivyo ni kuiepusha jamii na taifa kwa jumla katika maafa makubwa ya kufanya mitendo viovu.

Amefahamisha kwamba Zanzibar inahistoria kubwa katika kufuata mila na tabiaa njema zinazotokana na muongozo wa dini na kwamba bila jamii kujitahidi kwaelea vyema vijana upo uwezekano wa ladha na harufu njema ya kimaadili ya Zanzibar kupotea.

Hata hivyo ameupongeza uongozi wa Madrasa hiyo kwa jitihada kubwa za kuwalea  watoto kupitia misingi ya quran pamoja na kuwa na utaratibu mzuri wa kusimamia madrasa hiyo jambo ambalo linakosekana katika taasisi nyingi za namna hiyo hapa Zanzibar.

Naye Naibu Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Othman Ame Chum akimkaribisha Mhe. Othman kufungua Mkutano huo amesema kwamba Zanzibar inavipaji  vingi vya watoto na kwamba walimu waendelea na kazi kubwa ya kuvilea na kuvikuza vipaji hivyo.

Amesema changamoto ya ukosefu wa maadili iliyopo Zaanzibar kwa vijana kuyjiingiza kwenyer vitendo viovu kama vile vya utumiaji wa madawa ya kulevya , udhalilishaji dawa yake sio kuwepo sharia kali pekee bali ni pamoja na kuwajenga watoto na jamii kwa jumla katika maadili mema.

Akisoma Risala hiyo mbele ya Mgeni rasm Maalim  Rashid Sinan alimema kwamba pamoja na madras kutoa masheikh na waaalimu kadhaa lakini imekabiliwa na changamoto mbali ikiwemo vikalio, vifaa vya kufundishia kwa mfumo wa kisasa na kwamba waislamu ni muhimu kujitolea kusaidia madrasa ili dini ya kiislamu iweze kusonga mbele.

Imetolewa na ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia kitengo chake ha Habari leo tarehe 25.12.2022.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.