Habari za Punde

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu Zuhura Yunus azungumza na Wanahabari, Ikulu Jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu Zuhura Yunus akizungumza na kuwaelezea Waandishi wa Habari kuhusiana na Mafanikio ya ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan aliyofanya Davos nchini Uswizi tarehe 16-20 Januari,2023 pamoja na Dakar nchini Senegal tarehe 25-27 Januari, 2023 katika Mkutano uliofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 30 Januari, 2023.

Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusiana na Mafanikio ya ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan aliyofanya Dakar nchini Senegal tarehe 25-27 Januari, 2023 katika Mkutano uliofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 30 Januari, 2023.

Waandishi wa Habari wakiwa kwenye Mkutano uliohusu Mafanikio ya ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan aliyofanya Davos nchini Uswizi (tarehe 16-20 Januari,2023) pamoja na Dakar nchini Senegal tarehe 25-27 Januari, 2023. Mkutano huo wa Waandishi wa Habari umefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 30 Januari, 2023.

 

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.