Habari za Punde

Mhe Othman aitaka jamii kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman (wakatikati mwenye treki manjano) akishiriki katika mazoezi ya viungo na wanavikundi vya Mazoezi kutoka mikoa mbali mbali ya Tanzania Bara na Zanzibar baada ya kumaliza mazoezi ya kutembea yaliyoanza Muembe Kisonge na Kumalizikia Uwanja wa Amaan mjini Zanzibar leo tarehe 04. 02.03 .Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo chake cha Habari.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman akizungunza na wanavikundi vya Mazoezi kutoka mikoa mbali mbali ya Tanzania Bara na Zanzibar  baada ya kumaliza mazoezi ya kutembea yaliyoanza Muembe Kisonge na Kumalizikia Uwanja wa Amaani mjini Zanzibar leo tarehe 04.02.03. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar).

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman (mwenye treki manjano) akimkabidhi cheti cha Ushiriki Ernest Mosses kutoka kikundi cha Far East Joging group & Sport Club baada ya kushiriki katika mazoezi ya kutembea kuanzia  Muembe Kisonge na kumalizikia Uwanja wa Amaan mjini Zanzibar leo tarehe 04.02.2023.Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo chake cha Habari.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman (wakatikati mwenye treki manjano) akishiriki katika mazoezi ya kutembea pamoja na wanavikundi vya Mazoezi kutoka mikoa mbali mbali ya Tanzania Bara na Zanzibar yaliyoanzia  Muembe Kisonge na Kumalizikia Uwanja wa Amaan mjini Zanzibar leo tarehe 04.02.2023.Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo chake cha Habari.

MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, ameitaka jamii  kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi ili kusaidia kujenga afya na kuepusha nchi kutumia gharama kubwa kuwatibu wananchi kwa maradhi yasiyoambukiza.

Mhe. Othman ameyasema hayo huko uwanja wa Amaan  mjini Zanzibar alipozungunza katika Bonanzala kutumia miaka 18 tokea kuanzishwa kwa kikundi cha mazoezi cha Amani mjini Zanzibar baada ya kushiriki katika Matembezi ya mazoezi kuanzia Muembe Kisoinge  na kumalizikia uwanja wa Amaan ambayeo yalivishirikisha vikundi mbali mbali kutoka Zanzibar na Tanzania bara.

Amefahamisha kwamba kufanya mazoezi ni uwekezaji mkubwa kwa nchi na jamii  katika kutibu na kuweka kinga ya maradhi mbali mbali yatokanayo na mfumo wa ulaji na lishe isiyona mpangilio sahihi wa kitaalamu na kuchangia wananchi waliowengi kupata maradhi kama vile kisukari, sindikizo la damu na mengineyo.

Mhe. Makamu amesama kwamba serikali  kupitia tasasisi zake mbali mbali inaunga mkono jitihada za wananchi wanaojitokeza katika kujumuika kwenye mazoezi  mbali mbali jambo ambalo ni muhimu kwa afya zao na kupunguza gharama za matibabu kwa taifa.

Mhe. Othman amewataka wananchi kuhakikisha kwamba wanajenga utamaduni wa kupima afya zao kwa angalau mara moja kwa mwaka jambo ambalo litasaidia kujua hali zao na kuwa na thahadhari juu ya kujikinga na maradhi yatokanayo na vyakula hasa vya mafuta na sukari katika kiwango kikubwa kuliko inavyohitajika.

Aidha Mhe. Othman amewataka wananchi hasa wenye umri kubwa kuhakikisha kwamba wanaacha kula kwa wingi vyakula  vya mafuta mengi ikiwemo unywaji wa supu za makongoro na mengineyo ambayo yanaweza kuleta madhara kwa afya zao.

Mhe. Makamu amewapongeza wanavikundi hao na kuwataka kuhakikisha kwamba wanafanya juhudi kubwa za kujenga uelewa kwa jamii ili wananchi waliowengi waweze kushiriki katika mazoezi  ya aina mbali mbali ili kulinda afya zao na kujiepusha na maradhi mbali mbali.

Naye Mwenyekiti wa Klabu ya Mazoezi ya Amaan ndugu Ibarahim Chagua Abdalla, amesema kwamba Klabu hiyo imepata mafanikio makubwa kwa wanamicho kupunguza unene na kutoa wito kwa wananchi katika maeneo mbali mbali kujiunga na vikundi tofauti vya mazoezi ili kuisaidia taifa katika kupambana na maradhi yasiyoambukiza.

Katika risala yao ya wanamazoezi wa Klabu ya Amaan iliyosomwa ndugu Asmahani Yahya, amesema kwamba klabu hiyo, mbali na kufanikiwa katika kuendeleza shughuli za mazoezi, lakini pia imekuwa ikijitolea katika kusaidia shughuli mbali mbali za kijamii ikiwemo utoaji wa damu kuwasaidia wagonjwa.  

Katika mazoezi hayo yaliyoanzia Muembe Kisonge Mjini Unguja vikundi viulivyoshiriki vilitoka Mkoa wa Morogoro, Dodoama, Dar es Salaam na wenyeji Zanzibar viliongozwa na Klabu ya mazoezi kutoka Amani mjini Zanzibar.

Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo chake cha Habari leo tarehe 04.02.2023

 


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.