Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akizungumza
na wananchi wa eneo Pandambili mara baada ya kutembelea eneo ilipotokea ajali ya gari usiku wa kuamkia leo Alhamisi
Februari 9, 2023 na kusababisha vifo vya watu 12 na kujeruhi wengine 63. Wengine katika picha ni Mkuu wa
Wilaya ya Kongwa Remidius Mwema na viongozi wa Jeshi la Polisi.
Mkuu wa
Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akiwajulia hali majeruhi waliolazwa
katika Kituo cha Afya Gairo. Watu
12 wamefariki dunia na wengine 63 wamejeruhiwa katika ajali ya gari iliyotokea
usiku wa kuamkia leo Alhamisi Februari 9, 2023 wilayani Kongwa mkoani Dodoma imehusisha
gari aina ya Lori lenye namba za usajili T 677 DVX na basi la
abiri Kampuni ya Frester lenye namba za usajili T
415 DPP lililokuwa likitokea Bukoba kwenda Dar es Salaam.
Na.Lulu Mussa -- Pandambili, Dodoma.
Watu 12 wamefariki dunia na wengine 63 wamejeruhiwa katika ajali
ya gari iliyotokea usiku wa kuamkia leo Alhamisi Februari 9, 2023 wilayani
Kongwa mkoani Dodoma.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amesema kuwa ajali
hiyo imehusisha magari mawili na kusababisha vifo vya watu 12 (wanaume 8,
wanawake 4) na Majeruhi 63 (wanaume 40 wanawake 20).
Ajali hiyo imetokea usiku katika Kata ya Pandambili Kijiji cha Silwa
wilayani Kongwa, barabara ya Dodoma - Morogoro.
Majeruhi wanaendelea na matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya
Kongwa na Kituo cha Afya Gairo. Miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali
ya Wilaya ya Mkoa wa Morogoro na majeruhi 2 wamehamishiwa Hospitali ya Rufaa ya
Mkoa wa Dodoma.
“Ajali hii imetokea majira ya saa 6 usiku na imehusisha gari aina ya Lori lenye namba za usajili T 677 DVX na basi la abiri Kampuni ya Frester lenye namba za usajili T 415 DPP lililokuwa
likitokea Bukoba kwenda Dar es Salaam”.
Mkuu wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi Kamishna Awadh Haji ametaja chanzo cha ajali hiyo kuwa ni mwendo kasi na
uzembe wa dereva wa basi kutaka kulipita gari la mbele bila ya kuchukua tahadhari
na kugongana na Lori lililokuwa limebeba saruji.
Akizungumza na wakazi wa Pandamili eneo la ajali Mkuu wa Mkoa wa
Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ametoa rai kwa jamii kutii sheria bila shuruti
ili kuepuka ajali.
"Serikali ilikuwa na nia njema ya kuruhusu vyombo vya
usafiri kutembea usiku, lakini sasa baadhi ya madereva wanaanza kutozingatia
Sheria za usalama barabarani, tutaendelea kuwachukulia hatua kali’’ Alisisitiza
Mhe. Senyamule.
Awali Mkuu wa Mkoa wa Dodoma amewatembelea majeruhi katika Hospitali ya Kongwa na Kituo cha Afya Gairo kutoa pole na kuwatakia uponyaji wa haraka.
No comments:
Post a Comment