Habari za Punde

Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi Ahutubia Siku ya Wanawake Duniani Ukumbi wa Sheikh.Idrissa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar

Mke wa Rais wa Zanzibar Mhe.Mama Mariam Mwinyi  pia Mwenyekiti wa Taasisi  ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) (kushoto) akisalimiana na Viongozi wakati alipowasili katika viwanja vya Ukumbi wa Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar kushiriki katika Kongamano la Siku ya Wananwake Duniani lililofanyika leo,lililoandaliwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA)
Mke wa Rais wa Zanzibar Mhe.Mama Mariam  pia Mwenyekiti wa Taasisi  ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) (kulia) akifuatana na Mkuu wa Wilaya ya Magharibi "B" Mhe.Hamida Mussa Khamis  wakati alipowasili katika viwanja vya Ukumbi wa Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar kushiriki katika Kongamano la Siku ya Wananwake Duniani lililofanyika leo,lililoandaliwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA)
Naibu Kamishna wa Mamlaka ya Bima Tanzania (TIRA) Bi.Khadija Issa Said, alipokuwa akisoma taarifa yake katika Kongamano la Siku ya Wanawake Duniani, lililoandaliwa na  (TIRA) na kufanyika leo katika Ukumbi wa Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi pia Mwenyekiti wa Taasisi  ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) (kulia) alipokuwa akitoa hutuba yake leo katika Ukumbi wa Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar katika Kongamano la Siku ya Wanawake Duniani, lililoandaliwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA)

MWENYEKITI wa taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) na Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Bazaraza la Mapinduzi, Mama Mariam Mwinyi amewaasa wanawake nchini kulipa kipaumbele cha pekee suala la malezi ya watoto licha ya jitihada zao za kujitafutia riziki kwenye harakati zao za maisha.

Alisema jamii ya wanawake wengi imekubwa na taharuki ya kukimbizana na harakati za uchumi na kujitafutia maisha huku jukumu la ulezi likipewa mgongo hali aliyoieleza inaathiri sana watoto kwenye ustawi wa makuzi yao bila ya uwepo wa mama karibu.

Mama Mariam Mwinyi aliyasema hayo kwenye ufunguzi wa kongamano la siku ya Wanawake duniani lililofanyika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdul Wakil, Kikwajini wilaya ya wijini, Mkoa wa Mjini Magharibi.

Alisema mwanamke ana wajibu mkubwa wa ulezi wa familia na jamii katika mipango yake yote anayojipangia lazima atenge muda kwa ajili ya watoto wake.

“Katika mipango yote tunayoipanga lazima tuhakikishe tunalizungumzia suala zima la nafasi ya malezi kwa mwanamke, tunapokimbizana sana na uchumi katika miaka hii ya karibuni pametokea mwanya wa malezi kwa watoto, lazima tutenge muda kwaajili ya watoto wetu haijaalishi nafasi gani mwanamke yupo kwenye karakati zake, uwe Waziri au Mkurugenzi tuhakikishe watoto tunawapa nguvu na tunawaelekeza. Aliasa mama Mariam Mwinyi.

Alisema wanawake wako kwenye sekta zote za uchumi, wanafanya kila linalowezekana kwaajili matunzo ya familia zao.

Alisema katika harakati za kukabiliana na usawa wa kijinsi na kujikwamua kiuchumi kwa hali zote, wanawake wamekuwa wamebanwa na harakati hizo hivyo aliwaeleza kujua wajibu wao wa ulezi kwa watoto wao.

“Tusije tukakimbizana sana hili jambo la malezi tukalisahau sababu mwalimu wa kwanza duniani kwa mtoto ni mama, ni sisi ndio tunaobaki nao majumbani, mama ndie rafiki bora kwa mtoto, mama ni daktari wa kwanza nyumbani, duniani kwa mtoto ni mama, mama ndie anaetoa huruma kwa watoto wake, mtoto akiumia pale unapomwambia pole mwanangu, anapata hisia mama ndio kila kitu kwake, lazima tujichanganye kwenye muda wa kutafuta wakati huo huo ulezi wa familia.” Alisisitiza Mama.

Alisema kauli mbiu ya siku ya wanawake duniani mwaka 2023 inachanganua na kuwasisitiza wanawake wawe wadadisi, wajasiri, wajasiriamali na wabunifu na wenye kuleta mabadiliko yatakayo kabiliana na umasikini, haki, ukosefu wa kipato kwa jamii na taifa kwa ujumla kwa kutumia njia sahihi za teknolojia.

Aidha, Mama Mariam Mwinyi aliwashauri wanawake na kinamama kujitahidi kutumia fursa zinazopatikana kupitia teknolojia ya kisasa kwa kijitangaza kibiashara na kutumia soko la kimtandao kwajili ya kutangaza bidhaa na kazi za vikundi vyao ili kupata maendeleo ya haraka.

Pia, aliwashauri wazazi na walezi majumbani kuwashauri na kuwanasihi watoto wapende sana masomo ya sayansi ili kuwajenga mapema kuwa watoto wazuri wa teknolojia ya baadae, kwa kuwaungamkono na kuwasaidia kwenye masomo ya sayansi na hesabati badala ya kuwaachia na kuwa watoto wakawaida.

Alisema wazazi/walezi wanapaswa kutumia kigezo cha Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan kuwa kigezo bora kuzifikia ndoto za watoto wao kwa kuwapa moyo ili nabidii kwenye masomo yao ili waje wafuate nyayo za Rais Samia.

Alisema Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar inaunga mkono matumizi ya teknolejia kwa kuweka miundombinu bora ya teknolojia kwenye madarasa ya shule za msingi ili kuwajenga mapema watoto kiteknolojia.

Akizungumzia umuhimu wa bima, Mama Mariam Mwinyi aliitaka jamii kuona umuhimu wa kukata bima kwaajili ya kujikinga na majanga. Aidha, aliwataka Mamala ya Usimamizi wa Bima Tanzania TIRA kuongeza bidii ya kutoa miongozo na elimu kwa umma juu ya umuhimu wa kuwa na BIMA nchini.

Akizungumza kwenye hafla hiyo kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Uchumi, Dk. Sada Mkuya Salum, Naibu wa Wizara hiyo, Ali Suleiman Mrembo alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania zinadhamira njema kuhakikisha usawa wa kijinsia unakwenda sambamba kwenye kuleta maendeleo ya Watanania wote.

Alieleza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, imeelekeza mipango na sheria, miongozo na taratibu zake kuona usawa wa jinsia kwenye teknolojia unakuwa chachu ya ukombozi wa wanawake.

Naye, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Watoto, Ana Anatasi Paul, aliwashauri wanawake kupitia vikundi vya wajasiriamali na kinama kuitumia teknolojia kwa kujitangaza na kujitoa kiuchumi. Alisema wanawake walio wengi bado wako nyuma na matumizi ya tenkolojia, aliwashauri kuitumia fursa hiyo kujikwamua kiuchumi na kutangaza biashara zao na kulitumia vyema soko la teknolojia.

Kwa upande wake, Naibu Kamishna wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA), Khadija Issa alisema mafanikio ya shirika hilo yalichangiwa na ubunifu wa elimu jumuishi pamoja na njia za kisasa za usambazaji wa bima aidha, alieleza malengo ya Mamlaka hiyo kwa kushirikiana na wadau wake ikiwemo kutoa elimu kwa umma, kunzisha na kutekeleza mpango wa bima ya kilimo, uimarishaji na uunganishaji wa mifumo ya taasisi mbalimbali za serikali zikiwemo jeshi la polisi mamlaka za bandari, mamlaka zote za mapato nchini.

Pia, aliiomba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuipa ushirikiano mamlaka hiyo kwenye kutekeleza malengo yake hayo.

Kongamano hilo la siku ya wanawake duniani lilitayarishwa na Mamkala ya Usimamizi wa Bima, Tanzania, TIRA.

Wake wa Viongozi wastaafu na Mama Fatma Karume (kulia) wakijumuika katika na Wanawake mbali mbali katika Kongamano la Siku ya Wanawake Duniani, lililoandaliwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA),lililofanyika leo katika Ukumbi wa Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar.
Washiriki wa Kongamano la Siku ya Wanawake Duniani, lililoandaliwa na  (TIRA) wakimsikiliza Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi pia Mwenyekiti wa Taasisi  ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) (hayupo pichani) alipokuwa akitoa hutuba yake leo katika Ukumbi wa Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar
Washiriki wa Kongamano la Siku ya Wanawake Duniani, lililoandaliwa na  (TIRA) wakimsikiliza Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi pia Mwenyekiti wa Taasisi  ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) (hayupo pichani) alipokuwa akitoa hutuba yake leo katika Ukumbi wa Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi pia Mwenyekiti wa Taasisi  ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) alipokua akipokea mfano Hundi ya Shilingi za Kitanzania Millioni Ishirini kutoka kwa  Naibu Kamishna wa Mamlaka ya Bima Tanzania (TIRA) Bi.Khadija Issa Said zilizotolewa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania  (TIRA)  katika Kongamano la Siku ya Wanawake Duniani, lililofanyika leo katika Ukumbi wa Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam  pia Mwenyekiti wa Taasisi  ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) akipokea zawadi kutoka kwa Naibu Kamishna wa Mamlaka ya Bima Tanzania (TIRA) Bi.Khadija Issa Said,katika Kongamano la Siku ya Wanawake Duniani, lililoandaliwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) katika Ukumbi wa Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi  pia Mwenyekiti wa Taasisi  ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) akimsalimia Mke wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Mama Fatma Karume (katikati) aliyeshiriki katika Kongamano la Siku ya Wanawake Duniani, lililoandaliwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) katika Ukumbi wa Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar,(kushoto) Naibu Kamishna wa Mamlaka ya Bima Tanzania (TIRA) Bi.Khadija Issa Said.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.