Habari za Punde

Tahadhari Yatolewa Matumizi ya Maji ya Mchemchem ya Msuka -Mhe. Mazrui

Na Rahma Khamis Maelezo Zanzibar               5/4/2023

Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Nassor Ahmed Mazrui akizungumza na Waandishi wa Habari wakati alipokua akitoa Taarifa ya tahadhari kwa umma kuhusu  maji ya chemchem yanayodaiwa kuwa ni tiba yaliyopo pembezoni mwa Bahari  Shehia ya Msuka Mashariki Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba, huko Afisini kwake Mnazimmoja Mjini Unguja.
Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Nassor Ahmed Mazrui akizungumza na Waandishi wa Habari wakati alipokua akitoa Taarifa ya tahadhari kwa umma kuhusu  maji ya chemchem yanayodaiwa kuwa ni tiba yaliyopo pembezoni mwa Bahari  Shehia ya Msuka Mashariki Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba, huko Afisini kwake Mnazimmoja Mjini Unguja
Mkemia Mkuu wa Serikali Dkt.farid Mzee Mpatani  Akitoa ufafanuzi wa kitaalamu kwa Waandishi wa Habari  kuhusiana na maji ya chemechem yaliyopo pembezoni mwa Bahari,Shehia ya Msuka Mashariki Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba wakati  wa Mkutano na Waandishi hao uliolenga tahadhari juu ya maji hayo yanayodaiwa kuwa ni tiba, hafla iliyofanyika  huko Wizara ya Afya Mnazimmoja Mjini Unguja . April 05 , 2023.PICHA NA FAUZIA MUSSA –MAELEZO ZANZIBAR



Na Rahma Khamis Maelezo Zanzibar               5/4/2023
Wizara ya Afya Zanzibar imewataka wananchi kuacha kutumia maji ya chemchem yanayodaiwa kuwa tiba kwa maradhi mbalimbal ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza katika jamii.
Akitoa taarifa ya tahadhari kwa Waandishi wa Habari kuhusiana na maji hayo  huko Ofisini kwake Mnazimmoja Waziri  wa Afya Zanzibar Mhe,Nassor Ahmed Mazrui amesema kuwa maji hayo si salama na hayafai  kwa matumizi ya viumbe hai.
Amesema kuwa hivi karibuni kupitia mitandao ya kijamii kumekuwa kukisambaa taarifa ya kuwepo kwa chemchem ya maji katika shehia ya Msuka Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba, ambayo wanadai kuwa maji hayo ukinywa yanaweza kutibu  magonjwa mbalimbali
Aidha amesema kutokana na hali hiyo kumepelekea kujitokeza watu mbalimbali kutoka Pemba na nje ya hapo kuchukua maji hayo kwa kutumia vyombo mbalimbali ikiwemo madumu na chupa ambapo Wizara baada ya kusikia hivyo ilipeleka watalamu kuchukua sampuli ya maji hayo na kuyafanyia uchunguzi.
Amefahamisha kuwa uchunguzi umebaini   maji hayo sio salama na hayafai kwa matumizi ya binadam   kutokana na kuwa    na idadi kubwa   ya vimelea  kati ya 220 hadi 1800 kwa kila lita moja ya ujazo wa maji, kiasi ambacho kinasababisha maradhi ya kuharisha nas vidonda vya tumbo.
Pia amesema katika uchunguzi huo kumeonekana uwepo wa kloraid kiasi cha miligram1490hadi   2059  kwa kila lita moja ya maji kiwango ambacho ni kikubwa kwa matumizi ya Binadamu.
 Waziri Mazrui alifafanua kuwa kwa kawaida maji ya kunywa yanatakiwa yawe na kiasi cha chumvi kiwango 0 ambapo katika uchunguzi maji hayo yamebainika kuwa na Ukali wa chumvi kati ya 2.8 na  3.8 ambacho ni zaidi ya kiwango kilichokubalika kwa matumizi ya kunywa.
Aidha amefahamisha kuwa kutokana na matokeo hayo katika maji kunmeonesha kuwa maji hayo yamechafuliwa na kinyesi cha viumbe hai na kuwa na kiwango kikubwa cha kemikali ambacho sio salama katika mwili wa binadamu.
Waziri Mazrui amewataka Wananchi  waliotumia maji hayo kujitokeza katika vituo vya Afya kwa Ajili ya Uchunguzi zaidi.
"Ikiwa kutajitokeza matatizo yoyote kwa mtu amabae katumia maji hayo na amehisi mabadiliko katika mwili wake basi afike Hospitali mapema na sisi tutamfanyia uchunguzi na kumpatia tiba  bila ya gharama yeyote," alisema Waziri.
Akitoa ufafanuzi wa kitaalamu  Mkemia Mkuu wa Serikali Dokt, Farid Mzee Mpatani amesema ili maji yawe salama lazima kuangalia ubora wa nadharia ,kemikali za maji na vijidudu ambavyo vimo ndani maji ili kuhakikisha kuwa yapo salama kwa matumizi ya binadamu.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.