Makamu wa
Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman ( kulia) akizungunza na
Katibu Mtendaji wa Taasisi ya Mpango wa Hiari ya kujitathimini katika masuala ya
Utawala Boara Afrika ( APRM), Bwana
Lamau Mpolo huko ofisini kwa Makamu Migombani mjini ZANZIBAR leo tarehe
22 Agosti 2023. ( Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar)
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman , amesema kwamba kuwepo kwa Taasisi ya Kujitathmini kwa hiari Afrika katika masuala ya Utawala Bora ni fursa muhimu ya kusaidia kukuza uchumi na maendeleo endelevu nchini.
Mhe. Othman
ameyasema hayo ofisini kwake Migombani mjini Zanzibar alipokutana na kufanya
mazungumzo na ujumbe wa Taasisi hiyo kutoka Tanzania Bara uliongozwa na Katibu
Mtendaji wake Bwana Lamau Mpolo.
Mhe. Othman
amesema kwamba taasisi hiyo inapaswa kuelekeza juhudi zake kwa kuangalia kasoro na mapungufu kwenye masuala mbali mbali katika kuchangia kasi ya uwajibikaji ili
kuimarisha uchumi na kuiwezesha nchi kuondoka mahali ilipo sasa na kuweza
kusonga mbele kimaendeleo.
Amefahamisha
kwamba masuala yanayohusishwa na taasisi hiyo ya kujitathimini katika suala la utawala bora yanagusa uwajibikaji
kwa viongozi na wananchi ni muhimu hasa kwa vile yanazingatia maeneo
yote ya kiuchumi na kimaendeleo kwa taifa na jamii kwa jumla .
Amesema katika
kuunga mkono juhudi hizo ni lazima taasisi hiyo kupewa umuhimu stahiki kutoka
kwa jamii watendaji na serikali kwa jumla ili iweze kuakisi vyema mahitaji na
mipango bora ya maendeleo kwa nchi kwa kuwa masuala hayo yanamchango mkubwa
katika maendeleo ya nchi.
Amesema
kwamba iwapo masuala hayo yatapewa umhimu unaostahiki inawezekana ndani ya
Tanzania kuwepo matokeo chanya ya kimaendeleo kwa taifa katika kuleta
mabadiliko ya kiuchumi na taifa kuweza
kupiga hatua kama ilivyofanyika katika nchi mbali mbali duniani.
Aidha amesema kwamba masuala hayo yanapopewa msukumo stahiki pia yanachangia kuimarisha mahakama zenye ufanisi mkubwa ambazo ni moja kati ya nyenzo kubwa za kiuchumi na maendeleo.
Amefahamisha
kwamba nchi mbali mbali zenye mahakama zinazowajibikaji kwa ufanisi zimechangia
sana mataifa hayo kuweza kupiga hatua katika kukuza uwekezaji kwenye sekta na
maeneo mbali mbali na hivyo kuimarisha
upatikanaji wa mapato na kukuza uchumi wa nchi zao jambo ambalo linaweza
kutumika pia kwa Tanzania na ikaweza kupiga hatua.
Aidha Mhe.
Othman amesema kwamba iwapo masuala hayo yatasimamiwa ipasavyo yatasaidia sana katika
kurejesha imani kwa wananchi kwa kuwa
viongozi pia watasiamia maadili na kuitaka taasisi hiyo kuzitangaza kwa
wananchi shughulizao mbali mbali wanazofanya
ili kujenga uwelewa bora kwa umma.
Kwa upande
wake Katibu Mtendaji wa Taasisi hiyo ya Mapngo wa hiari wa kujitathimini katika
masuala ya utawalabora na demokrasia Afrika nchini Tanzania Lamau Mpolo amesema
kwamba Taasisi hiyo ni muhimu na inaendelea na jitihada za uratibu katika dhana
ya utawala bora kwa kuonesha kasoro na kutoa mapendekezo juu ya namna ya
kufanya marekebisho katika maeneo mbali mbali.
Amesema
kwamba hivi karibuni taasisi hiyo itapita kwa wananchi katika maeneo mbali
mbali ya Tanzania ili kusikiliza maoni hasa katika vigezo vya siasa , uchumi na
utawalabora ambavyo ndivyo vinavyotumika katika tathimi wanazozifanya.
Taasisi ya Mpango wa hiari ya kujitathmini katika
masuala ya utawala bora na Demokrasia
Afrika tayari imeridhiwa na nchi
43 kati ya 54 za Afrika yenye madhumuni ya kukuza dhana ya utawala bora kwa
kuzingatia vigezo vya ustawi wa kiuchumi
kwa jamii, siasa , Demokrasia ili kuleta
maendeleo endelevu.
Kitengo cha Habari
Ofisi ya
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar
Agosti 22,
2023.
No comments:
Post a Comment