Habari za Punde

Al hajj Dk. Hussain Amewanasihi Waumini wa Dini ya Kiislamu, Wazazi na Walezi Kwenye Jamii Kuhimiza Maadili Mema Kwenye Malezi ya Vijana Wao

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Wananchi wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, baada ya kumalizika kwa Kisomo na Dua Maalumu ya kumuombea yeye na Viongozi pamoja na Nchi, iliyoandaliwa na Wanazouni na Maimamu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja iliyofanyika katika Msikiti wa Markaz Fisabillilah Tablii Kidoti leo 3-9-2023


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Al hajj Dk. Hussain Ali Mwinyi amewanasihi waumini wa dini ya kiislamu, wazazi na walezi kwenye jamii kuhimiza maadili mema kwenye malezi ya vijana wao ili kulinusuru taifa na athari za mmong’onyoko wa maadili.

 

Al hajj Dk. Mwinyi aliyasema hayo Kiodoti Mkoa wa Kaskazini Unguja alikoshirirki dua  ya kuliombea taifa na viongozi wake.

 

Rais Dk. Mwinyi alihimiza malezi bora kwa jamii yanayoendana na mila, sila na tamaduni za asili ya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla yanayotokana na misingi ya dini ili kulinusuru taifa na athari za dawa zakulenya, udhalilishaji, wizi, uzembe, kubaguana na vijana waliokosa hofu ya kumuogopa Mwenyezi Mungu.

 

Pia, Al hajj Dk. Mwinyi alisifu hali ya amani, umoja, mshikamano na  maelewano iliopo nchini  na kuitaka jamii kuiendelea kuitunza,  pia ahimiza udugu na umoja uliopo bila kujali tofauti zao za kisiasa kwa kutekeleza shughuli za kijamii na kimaendeleo pamoja na kuwataka waumini wa dini ya Kiislamu kuendeleza utamaduni wa kuliombea dua taifa na watu wake.

 

“Ndugu zangu kila mara nasema na leo napenda nirudie tena katika mambo muhimu katika nchi yoyote, amani ni jambo la msingi na la kupewa umuhimu wa kipekee, nchi ikikosa amani hakuna jambo lolote linaweza kufanyika” alilisisitiza Al hajj Dk. Mwinyi.

 

Hata hivyo, Al hajj Dk. Mwinyi aliahidi kutimiza ahadi zote alizoziweka wakati uchaguzi kuu wa Zanzibar kwa wananchi pamoja na kuyatekeleza mambo muhimu yaliyokuwa hayako  kwenye ahadi zake nakueleza ni wajibu kwa viongozi kuyatekeleza kwa maslahi ya watu na taifa kwa ujumla.

 

Dua hiyo ya kuliombea taifa ilizishirikisha zaidi ya mardasa 700, viongozi wakuu wa dini, Serikali pampoja na vyama vya siasa.

 

IDARA YA MAWASILIANO IKULU, ZANZIBAR


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.