Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Mwinyi Amejumuika na Wananchi Katika Ibada ya Sala ya Ijumaa Msikiti Mkuu wa Ijumaa Miembeni Wilaya ya Mjini Unguja leo 13-10-2023bNA Mhe.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Viongozi wa Msikiti wa Ijumaa Miembeni Wilaya ya Mjini Unguja, alipowasili katika viwanja vya msikiti huo kwa ajili ya kujumuika na Wananchi wa Miembeni kwa ajili ya Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika leo 13-10-2023
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akimsikiliza Katibu Mtendaji wa Ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh. Khalid Ali Mfaume, baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Miembeni Wilaya ya Mjini Unguja leo 13-10-2023, na (kulia kwa Rais) Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Saleh Omar Kabi na (kushoto kwa Rais) Imamu wa Msikiti wa Miembeni Sheikh. Fahim Hafidh
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Waumini wa Dini ya Kiislam akiitikia dua ikisomwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Saleh Omar Kabi, baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa,iliyofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Miembeni Wilaya ya Mjini Unguja leo 13-10-2023.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Waumini wa Dini ya Kiislam akiitikia dua ikisomwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Saleh Omar Kabi, baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa,iliyofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Miembeni Wilaya ya Mjini Unguja leo 13-10-2023,na (kushoto kwa Rais) Imamu wa Skiti Mkuu wa Ijumaa Miembeni Sheikh. Fahim Hafidh
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Waumini wa Dini ya Kiislam, baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Miembeni Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar leo 13-10-2023. 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Al hajj Dk. Hussein Ali Mwinyi ameendeleza utaratibu wake wa kuwajuulia hali wazee na wananchi kwenye maeneo mbambali kwa kuwaombea dua na kuwatakia kheir na shufaa wagonjwa wapone haraka kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu.                                                                                                        

Alhaj Dk. Mwinyi amewatembelea Bw. Haji Ramadhan Suweid Buda, mwandishi wa habari mkongwe na mama mzazi wa Sheikh Samir Zulfikar wa Mahad el Juneid ya Mkunazini ambao wanaendelea na matibabu hospitali kuu ya Mnazi Mmoja.

Pia Alhaj Dk. Mwinyi aliwatembelea wazee wa Chama cha Mapinduzi ambao walitoa mchango mkubwa kwenye chama hicho akiwemo Bw. Kombo Mzee Kombo nyumbani kwake Miembeni Mkoa wa mjini Magharibi, Bw. Bora Afya Silima Haji nyumbani aliekua Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mjini Kichama nyumbani kwake Mwembelikunda na bi. Hiari Miraji Othman, Balozi wa nyumba 10 namba mbili huko nyumbani kwake Miembeni jitini.

Mapema, Alhaj Rais Dk. Mwinyi alijumuika na waumini wa dini ya Kiislam na wananchi wa Miembeni kwenye ibada ya sala ya Ijumaa kwenye msikiti wa Ijumaa, Miembeni, Wilaya ya Mjini.

Akizungumza kwenye ibada hiyo Katibu Mtendaji kutoka Ofisi ya Mufti Zanzibar, Sheikh Khalid Ali Mfaume aliwahimiza waumini wa Kiislam umuhimu wa tabia njema na kueleza kuwa tabia njema ni msingi wa mambo manne ikiwemo imani.

Sheikh Khalid alieleza kwenye tabia njema imani hudumu kwa kutekelezwa amri za Allah (S.W) pamoja na kufuatwa makatazo yake. Pia alieleza kukosekana kwa tabia njema imani hupungua na kuongezeka kwa vitendo vya kuporomoka kwa maadili ikiwemo kupungua kwa heshima kwenye familia na jamii.

Alisema siku hizi watoto hawawaheshimu wakubwa zao wakiwemo wazazi na walezi hata jamii zinazowazunguruka, aliiasa jamii ili kupunguza wimbi la ukosefu wa maadili na kuepusha athari kubwa za ndoa na takala zinazojitokeza kwenye jamii ni vyema kutafuta njia za busara ili kukinusuru kizazi cha sasa kilichogubigwa na wimbi la ukosefu wa heshima na maadili.

Pia aliiasa jamii kuendelea kuwafundisha mema watoto ili kukuza jamii yenye heshima na maadili mema na tabia njema.

Kwa upande wake, Khatib wa ibada hiyo ya sala ya  Ijumaa aliiasa jamii kwamba uzuri wa waumini na waislam ni elimu, adabu na kuheshimu viongozi na jamii inayowazunguruka kwa kujiepuka kutoa maneno yasiyofaa kwa viongozi, wazazi na jamii ili kujenga jamii iliyonjema.

IDARA YA MAWASILIANO, IKULU ZANZIBAR


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.