Habari za Punde

Rais wa Zanzibar nab Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Mwinyi Amezuru Kaburi la Rais Mstaaf wa Zanzibar Marehemi Sheikh.Idrisa Abdulwakil Kijijini Kwao Makunduchi

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi  amezuru kaburi la Rais Mstaafu wa Zanzibar Marehemu Sheikh Idrissa Abdulwakil  na kujumuika na Viongozi na Familia ya Marehemu  kumuombea dua iliyosomwa na Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Hassan Othman Ngwali, iliyofanyika katika kaburi la marehemu Kijijini kwao Makunduchi, wakati wa ziara yake katika Mkoa wa Kusini Unguja na kuhudhuria dua maalum ya kuwaombea Viongozi Wakuu na kuiombea Nchi Amani, dua hiyo iliyofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Mtegani Makunduchi na (kushoto kwa Rais) Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba,Sheria.Utumishi na Utawala Bora Zanzibar Mhe.Haroun Ali Suleiman na (kulia kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud na Mkuu wa Wilaya ya Kusini Mhe. Galos Nyimbo.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Viongozi na Familia ya Marehemu Sheikh Hassan Bin Ameir, alipofika katika kaburi la marehemu katika Kijiji cha Mtegani Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja, kwa ajili ya kumombea dua  ,akiwa katika ziara yake na kuhudhuria  dua maalum ya kuwaombea Viongozi Wakuu wa Nchi na kuiombea Nchi Amani,iliyofanyika katika msikiti Mkuu wa Ijuma Mtegani Makunduchi leo 16-12-2023.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.