Mratibu wa Programu ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya
Awali ya Mtoto kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na
Uratibu) Bi. Adela Mpina (Kulia) akifafanua jambo wakati wa
kikao cha Wataalam kutoka Oxford Policy Management,
Kushoto ni Mkururgenzi Msaidizi wa Idara ya Maendeleo ya
Watoto kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wanawake na Makundi Maalum tarehe 09 Mei, 2024 Jijini Dodoma.
Na Mwandishi wetu- Dodoma.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala
ya Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi amekutana na
kufanya mazungumzo na Wataalam kutoka Oxford Policy
Management kuhusu Uwezekano wa matumizi ya akili bandia
(Artificial Intelligence and Machine Learning) katika kufanya
mapitio ya matumizi ya umma (Public Expenditure Review).
Kikao hicho kimefanyika tarehe 09 Mei 2024 ofisini kwake
Jijini Dodoma ambapo Dkt. Yonazi amesema pia lengo la
kikao hicho ni kujadili kuhusu makuzi na maendeleo ya awali
ya mtoto (ECD) nchini Tanzania.
Ikumbukwe Serikali ya Tanzania ilizindua Programu ya Taifa
ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali yam Mtoto (PJT-
MMMAM) mwaka 2021 kama mpango mkuu wa kuzileta
pamoja Wizara na wadau mbalimbali ili kuboresha Makuzi na
maendeleo ya awali ya Watoto kuanzia kuzaliwa hadi umri wa
miaka 8.
No comments:
Post a Comment