Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameyasema hayo kwenye ufunguzi wa Kigoda Cha Taaluma cha Ukombozi na Maendeleo ya
Afrika cha Sheikh Abeid Amani Karume huko ukumbi wa Dk. Ali Muhammed Shein, Tunguu Wilaya ya Kati Mkoa wa
Kusini Unguja.
Alisema,
Serikali pia inatambua majukwaa kama hayo yapo mengi kwenye mataifa mbalimbali
duniani na kwa majina tafauti yamesaidia kufanikisha masuala ya kitaaluma na
maendeleo kupitia fani mbalimbali kwa tafiti, mijadala, maandiko na mapendekezo
kwa Serikali.
Vile vile
Dk. Mwinyi ameziomba taasisi binafsi na mashirika mengine ya ndani na ya
kimataifa, kushirikiana na Serikali kukisaidia Kigoda hicho kiendelee
kutekeleza majukumu yake.
Alisema, Mzee Abeid Amani Karume
alikuwa kiongozi shujaa, mzalendo aliyejitolea kuleta uhuru na maendeleo ya
Zanzibar na Afrika kwa ujumla baada yakuongoza Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
ya tarehe 12 Januari 1964, yaliyoleta uhuru wa kisiasa, kiuchumi na kijamii kwa
wananchi wa Zanzibar.
Akitaja Malengo ya kigoda hicho
Dk. Mwinyi alisema ni pamoja na kuhifadhi, kuibua na kueneza mawazo na fikra za
Sheikh Abeid Amani Karume kupitia tafiti, mijadala, makongamano, mikutano na
machapisho mbalimbali, pomoja na kuendeleza ushirikiano wa ndani na nje ya
Afrika ulioanzisha Sheikh Karume baada ya Mapinduzi.
Pia Dk. Mwinyi aliwanasihi wanataaluma
kutumia fursa ya kufanya tafiti na kazi nyengine za kitaaluma kupitia Kigoda
Cha Karume ili kustawisha taaluma zao na kuleta mchango kwa jamii ya watu wa
Zanzibar kwani matokeo ya tafiti zao yataisaidia Serikali kupanga mipango yake
ya maendeleo.
Wakichangia mada ya Mchango wa
Marehemu Mzee Abeid Aman Karume katika siasa za Zanzibar, Tanzania na Afrika
kwa ujumla, viongozi wastaafu, Dk. Jakaya kikwete, Dk. Amani Karume, Dk.
Ali Muhammed shein, na Mwanasiasa mkongwe na waziri Mstaafu wa Jamuhuri ya
Muungano wa Tanzania, Steven Masato Wasira walipongeza fikra, busara na maono
ya Mzee Karume kwenye ukombozi wa Zanzibar dhidi ya ukoloni na utumwa.
Dk. Jakaya Mwisho Kikwete, Rais
Mstaafu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania awamu ya nne kwenye hafla hiyo,
aliwataka Watanzania kuzitumia fursa za Maendeleo zilizopo baina ya pande mbili
za Muungano Zanzibar na Tanzania bara sambamba na kuzitunza, kuzilea,
kuziimarisha fikra za Mapinduzi na Muungano zilizoasisiwa na Viongozi waasisi
Marehemu Mzee Abeid Amani Karume na Baba wa Taifa, Hayati Julius Kambarage
Nyerere.
Alisema, kuanzishwa kwa kigoda cha
Mzee Abeid Amani Karume si heshima kwa Zanzibar pekee lakini kwa taifa zima la
Tanzania na tasnia yote ya Elimu nchini.
Naye, Balozi wa Kigoda cha Mzee
Karume na Rais Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar awamu ya Sita, Dk.
Aman Abeid Aman Karume ameipongeza Serikali kwa wazo la kuanzishwa Kigonda cha
Mzee Karume ili kuzienzi, kuzitunza na kuziendeleza fikra, busara na maono ya
Mzee Karume katika kuakisi Maendeleo makubwa yaliyofikiwa Zanzibar kwa
kurithishwa vizazi vya sasa na vinavyokuja.
Kwa upande wake, Rais Mstaafu wa
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar awamu ya Saba, Dk. Ali Muhammed Shein alisifu
uwezo wa Marehemu Mzee Karume hasa kuinua Sekta ya Elimu na utaalamu kwa
Zanzibar akiwa na lengo la kuijenga Zanzibar mpya kitaaluma.
Alisema, Mzee Karume alilifanikisha
hilo baada ya kutoa makundi ya Wazanzibari kuyapeleka kwenye mataifa ya kijamaa
barani Ulaya na Amerika ikiwemo, Cuba, China, Bulgaria, Urusi na mataifa
mengine kwa nia ya kujifunza na kurejesha Zanzibar uzoefu na Maendeleo ya
teknolojia.
Naye Waziri wa Elimu na Mafunzo ya
Amali Zanzibar, Ali Abdul Gulam Hussein, Akitoa shukurani zake baada ya kutawazwa
kuwa Mwenyekiti wa Kwanza wa Kigoda cha Mzee Karume, Prof. Egiland Pius Mihanjo alisifu
dhana ya Hayati Mzee Abeid Amani Karume ya “Mapinduzi daima” ni kuwa na
misingi imara, misukumo na mbinu bora za kuleta Mapinduzi ya Uchumi kwa
maendeleo ya Zanzibar.
Akichangia mada ya Mchango Mzee
Karume katika siasa za Zanzibar, Tanzania na Afrika, Mwanasiasa Mkongwe na
Waziri Mstaafu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Stephen Masato Wasira,
alisifu juhudi za Marehemu Mzee Karume kwa kisirikisha watu wakati wa uongozi
wake hasa kwenye harakati za ukombozi wa Zanzibar hasa alipounganisha vikundi vya
kijamii kuanzisha harakati za siasa kwenye miaka ya 1950 zilizofanikisha
Mapinduzi ya mwaka 1964.
IDARA YA MAWASILIANO, IKULU ZANZIBAR.
No comments:
Post a Comment