Na Abdi Shamnah
–WHUUM
WAANDISHI wa
Habari nchini, wameshauriwa kuandika habari zao kuambatana na nyanja maalum (speciallization) na kuondokana
na utamaduni wa kuandika habari katika nyanja zote.
Changamoto hiyo
imetolewa leo na Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Zanzibar, Said
Ali Mbarouk , wakati alipozungumza an waandishi wa habari kutoka Klabu ya
Uandishi wa Habari (Zanzibar Press
Club), pamoja na Menejiment ya Baraza la Habari Zanzibar, Tawi la Zanzibar
(MCT) katika ukumbi wa Ofisis za MCT zilizopo Mlandege.
Amesema katika
muelekeo wa baadae upatikanaji wa ajira katika tasnia ya habari, utapanuka sana
kupitia sekta binafsi, ambazo zitakuwa na mahitaji maalum.
Aliwataka
waandishi hao kujibidisha kitaaluma katika Nyanja mbali mbali, ikiwemo uchumi,siasa,
michezo, mazingira na nyenginezo ili
kuwa tayari kukabiliana na mabadiliko hayo.
Akiihusisha na
hoja hiyo, Waziri Mbarouk alisema hivi sasa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeelekeza
nguvu zake katika kufikia dhana ya ‘Utalii kwa wote’, hivyo ni muhimu kwa
waandishi wa habari kuwa na taaluma ya kutosha juu ya utalii, hivyo kuitaka
Press Club kujipanga vyema na kuwaandaa wanadishi wake katika muelekeo wa sekta
hiyo.
“Uwezo wa waandishi
wengi tulionao katika dhana ya uandishi wa habari maalum ni mdogo mno, MCT
saidieni kuona wanadishi wanakuwa na
taaluma ya kutosha na kuehgemea katika nyanja maalum ’, alisema Mbarouk.
Aliwakumbusha
waandishi hao umuhimu wa kuandika habari zilizo sahihi na zilizofanyiwa utafiti
wa kutosha ili kuepuka upotoshaji wa taarifa.
Aidha aliiomba MCT
kusimamia kimalilifu suala la maadili kwa waandishi wa habari kwa kigezo kuwa
litajenga mustakbali mwema kati ya wadau wa habari na jamii.
Katika hatua
nyengine Waziri huyo aliahidi kusaidia juhudi za kulipatia ufumbuzi tatizo la
ofisi linaloikabili klabu hiyo, kwa kigezo kuwa mahala ilipo sio muafaka kwa kazi
zilizokusudiwa.
Aidha alimtaka Katibu Mkuu wa Wizara yake
kuangalia uwezekano wa kuwapatia nafasi za mafunzo waandishi wa kujietegemea
(freelance), pale Wizara hiyo inapopata nafasi za masomo kwa waandishi wa
Serikali.
Mapema Mratibu wa
Baraza la Habari Zanzibar, Shifaa Said alimwomba Waziri Mbarouk kutoa msukumo
wa kuyashughulikia mapendekezo ya Baraza hilo juu ya uundwaji wa sheria za Habari.
Alisema kuna
miswada miwili ya mapendekezo ya wadau kuhusu sheria za habari, ikiwemo ule wa
Media Service Bill na ITI ambayo tayari
imewasilishwa Wizarani kwa kushughulikiwa kwa muda sasa.
Alisema sheria
hizo ni muhimu katika uhai na ustawi wa
fani ya uandishi wa habari hapa Zanzibar.
Mapema kwa nyakati
tofauti Waziri Mbarouk alipata fursa ya kuzitembelea taasisi za Press Club na
MCT na kupata maelezo mafupi juu ya utendaji wa kaz za kila siku.
No comments:
Post a Comment