Habari za Punde

Blog mpya ya wazanzibari wanaoishi nje yazinduliwa

Kifaa chengine kimeingia jamvini kuvinjari katika kutoa habari za Zanzibar


Kitembelee ukipata nafasi

Na Geofrey Kimbitikiri

Wazanzibari waishio nje na ambao jamaa zao walipoteza maisha yao na wengine kuathirika katika msiba wa kuzama boti ya MV Skagit, wamesikitika kwa kitendo cha aliyekuwa Waziri wa Mawasiliano na Miundombinu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ambae pia ni mwakilishi wa jimbo la Ole, wilaya ya Wete Mkoa wa kaskazini Pemba, Bw. Hamad Massoud Hamad, kwa kuwaomba radhi wapiga kura wake, wa jimbo la Ole kwa uamuzi wake wa kujiuzulu bila ya kuwaomba radhi wale jamaa waliopoteza ndugu zao katika msiba wa meli hio.

Kutokana na taarifa waliyoitoa kupitia Blog la Wazanzibari waishio nje liitwalo ZANZIBAR NI KWETU, Wazanzibari hao wamesikitika sana na kueleza kuwa wa kuombwa radhi walikuwa ndugu na jamaa ambao walipoteza maisha yao au kuathirika kwa kuzama meli hio ya MV Skagit.

" Kuomba radhi kwa kujiuzulu uwaziri baada ya makosa kutokea sio ukomavu bali ni siasa ya kikaragosi. Ingelikuwa vizuri kama Bw. Hamad angelifahamu kuwa wananchi hawamchagui Mwakilishi ili awe waziri. 

Kama Bw. Hamad angelijiuzulu uwakilishi hapo alikuwa mwenye sababu nzito ya kuwaomba radhi wapiga kura wake wa Ole, lakini sio kwa kujiuzulu uwaziri baada ya makosa kutokea chini ya uongozi wake. " walimalizia Wazanzibari hao kwenye taarifa yao fupi.



Source: www.zanzibarnikwetu.blogspot.com

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.