Habari za Punde

Bunge lajitosa mgogoro wa gesi Mtwara



Na Mwandishi wetu, Dodoma
SPIKA wa Bunge, Anna Makinda  ataunda Tume maalum itakayokwenda Mkoani Mtwara kusikiliza maoni ya wananchi kuhusu mgogoro wa gesi unaoendelea.
Akiahirisha kikao cha jana cha Bunge, Spika Makinda alisema tume hiyo itasikiliza wadau wote katika mgogoro huo ambao ni wananchi wa Mtwara ambao wanapinga gesi hiyo kutosafirishwa kwenda Dar es Salaam na serikali ambayo inataka kuchimba gesi hiyo na baadae kuisaifirisha hadi Dar es Salaam.
Alisema tume hiyo ambayo wajumbe wake watatangazwa baadae, itakuwa na kazi ya kukutana na wadau wote na baadae kuwasilisha ripoti yake kwake kwa ajili ya kujadiliwa na Wabunge.
Alisema ripoti ya suala hilo, itajadiliwa na kutolewa uamuzi kabla ya mkutano wa 10 wa bunge kumalizika.
Aliwataka wananchi wa Mtwara, kutoa ushirikiano kwa tume hiyo ikiwemo kueleza kwa uwazi kile ambacho wanakipinga ili bunge liweze kujiridhisha.

 
Wakati huo huo habari zilizotufikia zinasema serikali imekubali kilio cha wananchi wa Mtwara wanaotaka gesi inayozaliwasha mkoani humo isisafirishwe kupelekwa Dar es Salaam.

Uamuzi huo umefikiwa baada ya Waziri Mkuu kuongoza jopo la mawaziri sita kwenda Mtwara kutafuta suluhu ya kudumu kuhusiana na mgogoro huo uliodumu kwa muda mrefu sasa.

Sasa kiwanda cha kuchakata gesi kitajengwa mkoani humo na karibu megawati 900 za gesi zitakazozalishwa zitabakia mkoani humo, huku kiwango kidogo cha gesi kikisafirishwa kupelekwa Dar es Salaam.

Serikali  imetaja manufaa na faida ambazo wananchi wa Mtwara wanatarajia kuzipata kupitia mradi huo mkubwa.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene amesema mtambo mkubwa wa kusafishia gesi utajengwa mkoani humo.
Lakini alisema serikali pia itajenga viwanda vingine kadhaa, na ujenzi wa mtambo wa megawati 250 ambao utakuwa ukizalisha umeme na mwingine kujengwa mkoani Lindi eneo la Somanga Funga utakaokuwa ukizalisha megawati 520.




Akifafanua zaidi Simbachawene alisema eneo la Mikindani katika kijiji cha Msijute kinatarajiwa kujengwa kiwanda kikubwa cha saruji Afrika Mashariki na Kati chenye uwezo wa kutoai ajira kwa watu 6000 jambo ambalo ni manufaa ya Wanamtwara.
Alisema pia tayari kuna wawekezaji wa viwanda vya mbolea wamejitokeza kujenga viwanda mkoani Mtwara na serikali itaviacha vinu vya kuchimba na kusindika gesi eneo hilo jambo ambalo bado ni manufaa makubwa kwa wananchi.

“Viwanda vya kusindika gesi hii vimepangwa kujengwa maeneo ya Lubasi, Kishere, Mchinga Bay, Lindi, Sudi Bay, Airport pamoja na Mikindani, viwanda vyote hivi vitatoa ajira kubwa sana,” alisema.
Aidha aliongeza kuwa uzalishaji umeme wa kutosha kwa kutumia gesi utapunguza bei ya umeme na kuuzwa kati ya senti 6 na 8 za Marekani jambo ambalo litapunguza ugumu wa maisha na pia bei ya bidhaa nchini.

1 comment:

  1. kwakuwa watanganyika ndio imeundwa tume lkn kama wazanzibari basi wangepelewa wakurya kuwapiga mabomu. amakweli zanziba sinchi.

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.