Habari za Punde

Kesi 771 za ardhi zaripotiwa

Na Shemsia Khamis, Pemba
KESI za migogoro ya ardhi 771 zimeripotiwa katika mahakama ya ardhi mkoa wa kusini Pemba kuanzia mwaka 2006 hadi 2013.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Ofisa Mdhamini wizara ya ardhi kisiwani Pemba, Hemed Salum Hemed, alisema kati ya kesi hizo,kesi 555 tayari zimetolewa uamuzi.

Alisema kesi 261 ndio ziliozsalia katika mahakama hiyo, zikiwa katika hatua mbali mbali, ikiwemo kusikilizwa na kuitwa mashahidi.

Alisematokea kuanzishwa kwa mahakama hiyo, inaonekana migogoro inaongezeka siku hadi siku, kutokana na sababu mbali mbali, ikiwemo ardhi kupanda bei.

Kwa upande wake, Hakimu wa mahakama hiyo, Salum Hassan Bakar, alisema kuna changamoto kadhaa zinazowakabili katika kusikiliza kesi  za migogoro ya ardhi, ikiwa ni pamoja na mrundikano  wa kesi katika mahakama hiyo.


Akizungumzia athari zinazojitokeza kutokana na kuwepo kwa mogogoro ya ardhi katika jamii, alisema ni pamoja na kuongezeka chuki na hasama kwa wana jamii.

Nae  Karani wa mahakama hiyo, Seif Kassim Said, akitoa takwimu za kesi zilizoripotiwa mahakamani hapo, kuanzia mwaka 2011 hadi mwaka 2013 alisema jumla ya kesi 263 ziliripotiwa.


Alisema mwaka 2011 ziliripotiwa kesi 107, wakati mwaka 2012  ziliripotiwa kesi 61 na mwaka 2013 ziliripotiwa kesi 95.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.