Habari za Punde

Kikongwe auawa kwa kupasuliwa kichwa

Na Kadama Malunde,Kahama
MWANAMKE mmoja mzee mkazi wa Nyahanga,wilayani Kahama mkoani Shinyanga, Rebeka Shija  (82), ameuawa kikatili kwa kukatwa kwa shoka kichwani na mke wa mtoto wake, aliyejulikana kwa jina la Magreth Richard (30).

Walioshuhudia tukio  walisema limetokea jana majira ya saa 3:00 asubuhi katika mtaa wa Nyahanga, mjini Kahama ambapo marehemu Rebeka Shija alienda nyumbani kwa mtoto wake wa kiume, Bundala Sengasenga (46) alikokuwa ameitwa na mkwewe kumsaidia kuanika dengu.

Mashuhuda hao walisema marehemu alikuwa akiishi kwa mwanawe mkubwa, Stanley Sengasenga,katika mtaa huo.

Mtuhumiwa wa mauaji hayo, alisema mama mkwe wake alifikia sebuleni na kwamba wakati yeye yuko nje, alimwona mtu ambaye hakuweza kumfahamu akitoka sebuleni hapo na kukimbia  na alipoangalia alimkuta mkwewe akiwa ameuawa.

 Imeleelezwa kuwa kabla ya tukio, mtuhumiwa ambae  kwa sasa anashikiliwa na jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga kwa mahojiano,  alikwenda nyumba ya jirani yake aitwaye Noeli Mkisi kuazima shoka kwa ajili ya kuchanja kuni.

Hata hivyo, katika hali ya kushangaza shoka hilo baadaye lilikutwa kwenye shimo la maji taka nyumbani hapo.


 Imeelezwa kuwa shoka hilo lilipatikana baada ya mbinu za kiupelelezi za jeshi la polisi kuagiza gari la maji taka kuyavuta maji hayo baada ya majirani kudai hawajaona mtu aliyekimbia na shoka muda huo katika mwelekeo ambao mtuhumiwa alielekeza.

Kaimu Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga, Kamishina Msaidizi wa Polisi, Kihenya Kihenya alisema marehemu aliuawa kwa kukatwa shoka kichwani na mtuhumiwa ambaye ni mke wa mtoto wake.

Alisema baada ya mauji hayo mtuhumiwa alimuacha marehemu sebuleni kisha kutumbikiza shoka alilotumia kufanya unyama kwenye tenki la kuhifadhi  maji.

Alisema chanzo cha mauaji hayo ni imani za kishirikina.

Wakati huo huo mwanamme mmoja asiyejulikana jina wala makazi yake (25-30) amekutwa ameuawa kwa kushambuliwa kwa mawe.

1 comment:

  1. Aise watanganyika ni makatili. Yaani we acha tu. Hizi balaa zao wasituletee Zanzibar.

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.