Habari za Punde

Balozi Seif Afungua Maonesho ya 77 Dar.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akimkabidhi tuzo Maalum Mkuu wa Miradi wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii Tanzania { NSSF } Mhandisi Julius Nyamuhokya baada ya shirika lake kudhamini sherehe za ufunguzi wa maonyesho ya 38 ya Kimataifa ya Biashara ya Saba saba yaliyoanza rasmi jijini Dar es salaam.
Balozi Seif akiangalia mabomba ya kusambazia maji yaliyotengenezwa na shirika la mabomba Tanzania kwenye maonyesho ya 38 ya Kimataifa ya saba saba Jijini Dar es salaam.

Balozi Seif akiwa na mwenyeji wake Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania { Tan Trade } Bibi Sabetha Mwambenja akiingia ndani ya viwanja vya maonyesho ya saba saba ya Mwalimu j.k Nyerere kuyafungua maonyesho ya 38 ya Kimataifa ya Biashara.
Mkuu wa Miradi wa NSSF Mhandisi Julius Nyamuhokya akimpatia maelezo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif juu ya haraki za miradi yao ya ujenzi wa nyumba katika eneo jipya la Kigamboni.
Meneja mauzo wa shirika la Biashara  la la Taifa Zanzibar { ZSTC } Ndugu Issa Hamid akimpatia maelezo Balozi Seif kwenye banda la biashara la Zanzibar kwenye maonyesho ya 38 ya Kimataifa ya Biashara Jijini Dar es salaam.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akimuaga rasmi Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya maendeleo ya Biashara Tanzania { Tan Trade } Bibi SabethaMwambenja baada ya kufungua maonyesho ya 38 ya Kimataifa ya Biashara Dar es salaam.
(Picha na Hassan Issa wa – OMPR)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.