Habari za Punde

Kariakoo Amusement Park katika Sura Mpya Kufurahisha watoto, kuinua Uchumi na Ajira.

Na Waandishi wetu, ZJMMC.                                                                                                      
“Hivi unaweza kuamini kuna watu wanatoka Dar-es-salaam na kuja Zanzibar kwa ajili ya kufuata pembea?”

Ndugu Mussa Yussuf Mussa afisa habari mkuu wa mfuko wa hifadhi ya jamii Zanzibar, aliyasema hayo yalipofanyika mahojiano maalum katika ofisi za ZSSF(ZANZIBAR SOCIAL SECURITY FUND) makao makuu Kilimani, Manara wa Mbao Zanzibar.

Alianza mazungumzo yetu kwa kusema kuwa mnamo tarehe 3 Septemba, 2008. Serikali ya Mapinduzi Zanzibar chini ya Rais wa wakati huo Mh.Dk.Amani Abeid Karume, aliamuru viwanja vya Uhuru Kariakoo Amusement Park viwe chini ya usimamizi wa ZSSF. Baada ya baadhi ya wafanyabiashara kuomba vibinafsishwe kwao ili waviendeshe.
Alisema mwaka 2008 ZSSF walianza ukarabati mdogo wa viwanja hivyo vya kufurahisha watoto. Na vikaanza kazi kwa muda kukiwa na pembea tano. Kama Chairtour, Pembea ya farasi, Pembea ya vikapu na nyinginezo.

Alisema ZSSF wamepewa jukumu hili la kukiendesha kiwanja hicho likitoka  katika usimamizi wa Wizara ya Habari Utalii utamaduni na michezo tangu mwaka 1980 hadi ilipokabidhiwa rasmi kwa ZSSF mwaka 2008.

Alisema Historia ya viwanja hivi inatokana na sera za chama cha Afro-Shirazi (ASP) katika harakati zake za kustawisha hali za wananchi zifanane na pia kuwaangalia watoto wa wafanyakazi na wakulima.

“Iwapo ASP itakapopata  madaraka ya serikali itazingatia ustawi wa jamii katika hali iliyobora.” Afisa habari mkuu wa ZSSF bwana Mussa Yussuf Mussa alinukuu hali ilivyokuwa hapo zamani.


Alifahamisha kuwa baada ya kupata madaraka serikali ya chama cha ASP mwanzoni mwa miaka ya 1970 waliweza kutekeleza mambo mbalimbali katika kustawisha hali za wananchi kama kujengwa kwa majengo ya Michenzani yanayotumika kwa makazi hadi hii leo.Kusimamia ununuzi wa meli ya M.V Maendeleo, Mapinduzi na Ukombozi.

Ujenzi wa viwanja vya uhuru maarufu kwa jina la Kariakoo ulipewa jina hilo baada  ya kuwepo katika eneo la Kariakoo mjini Zanzibar.
Alieleza kuwa ujenzi ulianza  mwaka 1974 ukakamalika mwaka 1975 katika kipindi cha serikali iliyokuwa inaongozwa na Rais wa wakati huo Mh .Aboud Jumbe Mwinyi  ikisimamiwa chini ya halmashauri ya uingizaji zana za ujenzi.

“1976 kiwanja cha Kariakoo kilianza rasmi kazi ya kufurahisha watoto na watu wazima kukiwa na pembea saba,” alifahamisha.

Hata hivyo, Afisa huyo wa uhusiano wa ZSSF alieleza kuwa Kuna kipindi kiwanja kilipoteza umaarufu na kuchakaa, kutokana na usimamizi mbaya wa wakati huo; na hata suala la kugharamia uendeshaji wa kiwanja hicho ilishindikana.

“Enzi zile wananchi hawakuwa na jukumu la kulipia wanapoingia ndani ya kiwanja. Lakini sasa kutakuwa na gharama za kuingilia pia kutumia pembea. Hii itasaidia katika kumudu mahitaji ya uendeshaji pia kulipatia taifa pato lake ili kuleta maendeleo na ustawi uliobora kwa jamii,” alisema Mussa akionesha kuwepo usimamizi imara wa kukusanya mapato.

Alisema matumaini yameanza kurudi  baada ya miaka mitatu ya kufungwa kiwanja hicho kwa ajili ya ujenzi mpya na Sasa ujenzi umekamilika kwa asilimia tisini.

Alisema ZSSF imefanikiwa kutekeleza moja ya majukumu yake ya kuwekeza fedha zinazotokana na michango kwenye miradi yenye faida kama itakavyo idhinishwa na bodi ya wadhamini wa ZSSF.

Alisema katika mradi wa ujenzi wa kiwanja hicho cha watoto; Bilioni 13 zinakadiriwa zitatumika kukamilisha mradi huo, unaotarajiwa kukamilika mwezi January au februari  2015.

Alisema kampuni ya CRJE kutoka china iliingia mkataba na ZSSF 24 oktoba 2012 wa kandarasi ya ujenzi wa miundombinu. Pia kampuni nyingine ya GOLDEN HORSE imeingia mkataba kwa ajili ya kufunga mapembea.

“utakapo kamilika uwanja huo kutakuwemo na michezo mbalimbali kama video games, water slides na mapembea ya aina mbalimbali,” aliyasema hayo ndugu Abdallah Juma afisa habari ZSSF makao makuu.
“kuna kadiriwa kutakuwepo na pembea zipatazo 16. Kama vile 
Airbike, Gerry fish, Sky diver, Viking, Pambercar,Supersewingna nyinginenyingi,” aliongezea katika ufafanuzi wake ndugu Abdallah Juma.

Aidha alisema tarehe 26 Septemba,2014 haitosahaulika; kwani majaribio ya kutumika kiwanja kipya cha NEW ZSSF UHURU KARIAKOO AMUSEMENT PARK yalifanyika kwa muda wa siku 5. Na pembea zipatazo 12 zilitumika katika uzinduzi huo.

Mussa alisema ili kuhakikisha msaada wa haraka unaweza kupatikana endapo kama kutatokea tatizo lolote, ZSSF walifuata ushauri uliotolewa na rais wa serikali ya mapinduzi  Zanzibar Dk.Ali Mohamed.Shein kuzipatia ufumbuzi nyumba zote zilizogandamana na uwanja huo kwa kuzinunua.

“Ushauri wa mkubwa ni agizo,” alisema afisa habari mkuu wa ZSSF makao makuu.

Alieleza kuwa hivi sasa kiwanja kimekuwa na eneo la kutosha nje. Ndani hakuna majengo yaliyo kama tube ili kuepuka matatizo mbalimbali ya kimazingira kama magonjwa yanayosambazwa kwa njia ya hewa.

Akielezea mambo mengine alisema kutakuwemo na maduka yatakayouza vitu vya watoto kama toys,mkahawa wa chakula na ukumbi utakao tumika kwa mikutano, harusi, na shughuli mbalimbali.

“Tukumbuke hii ni sehemu ya kufurahisha watoto mambo yanayofaa katika eneo hili ni yale yatakayo endeleza furaha ya watoto. Hivyo haifai kuuzwa kwa vileo ama kuvitumia vitu kama sigara, bangi, viroba n.k. kwani matumizi ya mihadarati kwa uwazi mbele ya watoto itaharibu malezi na maadili yao”. alisema

Juu ya ajira alisema “Ajira tumezigawa sehemu kuu mbili skilled na unskilled. Hivi mfagiaji anahitaji elimu, pia kutakuwepo na ajira nyingine zitakazotokana na maduka tutakayo kodisha,” alifahamisha afisa habari mkuu ndugu Mussa Yussuf Mussa.

Alisema inakadiriwa kupatikana ajira maalum za moja kwa moja 50 ndani ya kiwanja hicho katika maeneo ya utawala, mafundi na wale watakao ongoza watumiaji wa pembea na michezo mbalimbali.

Kuhusu usalama alisema kuna CCTV kamera zenye uwezo wa kuchukua, kurekodi matukio mbalimbali ndani na nje ya uwanja; pia jeshi la polisi na vyombo vingine vya ulinzi vitasaidia kuhakikisha ulinzi unapatikana ndani ya kiwanja kwa kipindi chote cha michezo.

“Mabomba maalum ya kutolea matangazo yatakuwemo ya kutosha ili kurahisisha suala la kutoa matangazo mbalimbali pale yatakapo hitajiaka. Pia kuna milango ya dharura ya kutosha itakayotumika endapo litatokea jambo si la kawaida,” alifahamisha.

Akielezea huduma za kiafya alisema msalaba mwekundu, madaktari mahiri watatoa huduma za kiafya ndani ya kiwanja pindi mtu atakapo pata tatizo la kiafya, iwe kuanguka, kuumia na mengineyo.
“yeyote atakapopata tatizo la kiafya ndani ya kiwanja tutamshughulikia kwa kutumia wataalamu tuliokuwa nao, endapo tatizo litakuwa kubwa tutampeleka hospitalini kwa gharama zetu.” Alizungumza kwa msisitizo afisa habari mkuu wa ZSSF makao makuu.

Hata hivyo,ndug Abdallah Juma alisema idadi ya watu elfu sita inakadiriwa kuwa wataingia kwa wakati mmoja ndani ya kiwanja hicho kwa kujumuisha wale watakaokuwa wanatumia pembea na wanaotumia maeneo mengine.

“Kiwanja kinadhaniwa kitaweza kufanya kazi kwa muda wa siku 7 za wiki. Kitafungwa saa 3 usiku kwa siku za kawaida na saa 4 kwa siku za sikukuu kitakapoanza rasmi kazi,” alifahamisha namna kitakavyofanya kazi huku akisema jambo hilo bado halijadiliwa kwa kina hadi pale watakapo kabidhiwa, ndugu Mussa.

“Njia mbalimbali zitatumika kukitangaza kiwanja hicho ndani na nje ya Zanzibar kupitia traditional media, social media, blogs na word mouth”, aliongeza.

Alisema kiwanja hiki kitaongeza thamani ya visiwa vya Zanzibar katika sekta ya utalii pia kustawisha hali bora za wananchi katika michezo mbalimbali pia burudani. Alisema kitavutia sio tu kwa wakazi na wenyeji wa Zanzibar, lakini pia wale wanaotoka ndani na nje ya bara la Afrika.

“Zanzibar tumebarikiwa kuwa na sehemu mbalimbali za kupumzika na kufurahi kama jamuhuri garden, forodhani na kariakoo kwa unguja”, alisema

Hata hivyo, alisema si mradi huu wa NEW ZSSF UHURU KARIAKOO AMUSEMENT PARK pia upo mwingine unaoendelea katika ujenzi kisiwani Pemba kwenye uwanja wa UMOJA uliopo kwenye eneo la tibirinzi.

“Yatupasa tufahamu na tuzingatie kiwanja hiki kitakapo kamilika na kukabidhiwa rasmi kwa ZSSF ni mali yetu sote wakazi wa Zanzibar hatuna budi kukitunza kwa lengo la kutuburudisha , kujifunza, kuendeleza mahusiano bora kati ya jamii na taasisi za serikali,” alitahadharisha afisa huyo wa habari mkuu wa ZSSF.

Alisema ujenzi haujakamilika na watu wasiwe na wasiwasi kwa baadhi ya mapungufu yaliyojitikeza kipindi cha majaribio. na inshaallah kila kitu kitakamilika kama ilivyopangwa.

“kimejengwa kwa ajili yao; kitunze kidumu, suala la kukitunza tusiachiwe peke yetu,” alihitimisha mahojiano yetu kwa kauli hiyo ndugu Mussa Yussuf Mussa afisa habari mkuu ZSSF makao makuu.


Makala haya ya Imeandaliwa na HARUNA OMARY SAID mwanafunzi chuo cha habari Zanzibar anapatikana kwa namba 0659 526 004, 

Na kuhaririwa na MOHAMMED MZEE mwalimu chuo cha habari Zanzibar.

Shukrani ziwaendee.
1.      LUCAS ANDREW MKUI.
2.      ATIE ALI KHAMIS.
3.      MWAPILI VITUS.
4.      ALLY YAHAYA ALI.
5.      MARYAM RAJAB BAKAR.
6.      UMMUL-KULTHUMU IBRAHIM OTHMAN.
7.      HIDAYA KHAMIS MSHENGA.

Kwa kushirikiana nami katika kutafuta taarifa zote za muhimu za kukamilisha makala haya yaliyonichukua takribani saa 96 hadi kukamilika kwake huku nikikutana na changamoto nyingi za kunikatisha tama.
Pia shukrani kwa
1. 
     MASHA ALI MUSSA(Dada yangu na msimamizi wa kazi zangu)
2.      MWAJABU IDDI(Mama, kunitia moyo usiku na mchana kipindi nafuatilia mambo mbalimbali)
3.      THABIT MADAI(Kwa kunichangia mawazo kipindi naandika makala haya)
4.      ALI MASOUD(Kunisaidia ufundi wa laptop yangu kipindi chote bila kusita)
5.      Wanafunzi wa cheti chuo cha habari Zanzibar  2014/2015 kwa ushirikiano wao.

6.      MAKAME USSI SHOMARI(Mwl. Wa Kiswahili chuo cha habari Zanzibar )
7.      SALEHE R. KOSHUMA(Mshauri wangu mkubwa, mwl. Chuo cha habari Zanzibar )
8.      HANIFA
9.      YUSUF SIMAI ISSA(Mdogo wangu).

Nakusii endelea kumakinika nami katika muendelezo wa makala za mithili yako hapana na hatua zangu ndani ya mji mkongwe nikiangazia mambo mblimbali ya kijamii, kisiasa, uchumi na historia, burudani hata tamaduni.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.