Habari za Punde

Mkutano wa CCM jimbo la Dimani: CCM ndiyo chama kinachojali maslahi na maendeleo ya wananchi.


 Baadhi ya wanaCCM waliohudhuria katika Mkutano wa hadhara wa kampeni za CCM Jimbo la Dimani Mkoa wa Mjini Magharibi  Unguja wakimskiliza mgeni rasmi katika mkutano huo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akizungumza  nao leo katika uwanja wa mpira wa Dimani leo,[Picha na Ikulu.]  
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akiwahutubia wananchi na WanaCCM katika Mkutano wa hadhara wa kampeni za CCM Jimbo la Dimani Mkoa wa Mjini Magharibi  Unguja  katika uwanja wa mpira wa Dimani leo,[Picha na Ikulu.]
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akiwahutubia wananchi na WanaCCM katika Mkutano wa hadhara wa kampeni za CCM Jimbo la Dimani Mkoa wa Mjini Magharibi  Unguja  katika uwanja wa mpira wa Dimani leo,[Picha na Ikulu.]
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai akiwaombea kura Viongozi wa CCM walioomba nafasi za Uongozi katika kamapeni za CCM zilizofanyika leo katika uwanja wa mpira Dimani Wilaya ya Magharibi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Jimbo la Dimani,mgeni rasmi akiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shei,[Picha na Ikulu.]
 Maelfu ya Wananchama wa CCM na Wananchi waliohudhuria katika mkutano wa hadhara wa Kampeni za CCM Jimbo la Dimani Wilaya ya Magharibi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja wakimsikiliza  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein wakati alipozungumza nao leo,[Picha na Ikulu.]
 Maelfu ya Wananchama wa CCM na Wananchi waliohudhuria katika mkutano wa hadhara wa Kampeni za CCM Jimbo la Dimani Wilaya ya Magharibi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja wakimsikiliza  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein wakati alipozungumza nao leo,[Picha na Ikulu.]
 Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Dkt.Mohamed Seif Khatib alipokuwa akiwasalimia wanachama wa CCM na wananchi wa Jimbo la Dimani katika mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika le katika uwanja wa mpira Dimani Wilaya ya Magharibi Unguja,[Picha na Ikulu.]
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai akiwaombea kura Viongozi wa CCM walioomba nafasi za Uongozi katika kamapeni za CCM zilizofanyika leo katika uwanja wa mpira Dimani Wilaya ya Magharibi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Jimbo la Dimani,mgeni rasmi akiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shei,[Picha na Ikulu.]


  
STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar                          19.10.2015
---
VIONGOZI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamewaeleza wanaCCM na Wananchi kuwa hakuna chama chenye historia,kujali maslahi na maendeleo ya wananchi isipokuwa CCM hivyo kuna kila sababu ya wao kuwachagua viongozi wa chama hicho wanaogombania nafasi za uongozi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika mkutano wa Kampeni ya uchaguzi wa CCM uliohudhuriwa na maelfu ya wananchi na wanaCCM uliofanyika uwanja wa Mpira Dimani, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini Magharibi ambapo mgeni rasmin alikuwa mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Dk. Ali Mohamed Shein.

Nae Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Mohammed Seif Khatib alisema kuwa hakuna chama hata kimoja chenye historia ya ukombozi isipokuwa chama cha CCM ambacho kinawajali na kinawathamini wananchi.


Alisema kuwa CCM ina Sera thabiti kwani inayatambua na inayathamini Mapinduzi ya Januari 12, 1964 ambapo pia, chama hicho kimezaa Muungano ambao umeleta umoja na mshikamano hadi hivi leo.

Alisema kuwa CCM ina kila sababu ya kuingia Ikulu kwani mgombea wake wa Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM, Dk. Ali Mohamed Shein ana kila sifa, elimu ya juu ya Sayansi, ana Digirii tatu, mtu wa watu, mpole na myenyekevu na anawapenda Wazanzibari, si mbaguzi.

Nae Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Idd alisema kuwa uhuru wa Zanzibar umepatikana kutokana na wakulima na wakwezi hivyo hashangazwi na viongozi wa chama cha CUF kumwambia kuwa andapo watapa nchi akatafute jembe akalime.

Balozi Seif pia, alishangazwa na chama cha CUF kusema kuwa Zanzibar hakuna maendeleo na kueleza kuwa maendeleo yaliopo hivi sasa hawayaoni.

Balozi Seif alisema kuwa tayari kuna baadhi ya wafuasi wa chama cha CUF wameshadhamiria kufanya fujo na hivi sasa tayari wameshawahamisha watoto wao kuwapelekea Pemba ili wao wabakie kwa lengo la kufanya vurugu.

Alisema kuwa Chama cha CUF kimejiandaa kuwadhibiti wafuasi wa CCM siku ya uchaguzi na kueleza kuwa CCM imeshapata habari na vyombo vinavyohusika katika kusimamia amani na utulivu vitawashughulikia wale wote watakao leta vurugu.

Aidha, Balozi Seif alitumia fursa hiyo kuwaombea kura wagombea wote wa CCM.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai alitoa pongezi kwa wanaCCM kwa kushiriki vyema katika mikutano ya chama hicho na kueleza kuwa kuna kila sababu ya ushindi wa CCM.

Nae Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Magharibi, Yussuf Mohammed, alisema kuwa CCM itashinda kwa ushindi mkubwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Alisema kuwa uwanja wa mpira wa Bweleo umetengezwa na Serikali ya CCM na kushangazwa  na ahadi zilizotolewa na viongozi wa CUF kujenga uwanja huo ambapo ahadi hizo zote zilikuwa hewa na badala yake Serikali chini ya CCM umekijenga kiwanja hicho.

Alisema kuwa Mapadri, Maaskofu na Wachunganyi amani yao iko kwa CCM na sio chama cha CUF kwani chama hicho hawana imani nzuri na watu wa dini ya Kikiristo kutokana na maovu mbali mbali waliowafanyia watu wa dini hiyo hapa nchini.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.