Habari za Punde

Uzinduzi wa mradi wa maji safi Kinduni

Na Khadija Khamis –Maelezo      

Zaidi ya shilingi million 73 za Kitanzania zimetumika kwa ajili ya kufanikisha  mradi wa maji  safi na salama katika kijiji cha kinduni wilaya ya kaskazini B Unguja ambapo zaidi ya wananchi 5582 watafaidika na mradi huo.

Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Makaazi Maji na Nishati Ali Khalili Mirza ameeleza hayo mbele ya Waziri wa Kilimo na Maliasili Mhe.Dkt. Sira Ubwa Mamboya wakati wa  uzinduzi wa mradi wa maji  safi Kinduni ikiwa ni muendelezo wa shamrashamra za Sherehe ya Miaka 52 ya Mapinduzi Zanzibar .

Alisema fedha zilizotumika kwa kufanikisha mradi huo ni nyingi  hivyo iko haja kwa wananchi kuhakikisha wanalinda na kuenzi rasilimali hiyo ili iwe chachu ya kuleta maendeleo katika kijiji hicho na vijiji  vya karibu ambavyo vitafaidika na huduma  hiyo .

 Waziri wa Kilimo aliwataka wananchi wa vijiji hivyo  kujenga  mashirikiano katika kulinda na kutunza vianziao vya maji ili viweze kudumu kwa muda mrefu na kuondondosha  usumbufu wa tatizo hilo .


“Tone  moja la maji ni gharama  hivyo tunapaswa kuongeza ushirikiano  katika kulinda, kutunza na kudumisha rasilimali hiyo tuliopewa,“ Alisema Dkt. Sira .

Hata hiyo Waziri Mamboya aliwataka wananchi kuchangia  huduma hiyo   ili kukabiliana na gharama ndogo ndogo za uchakavu wa vifaa   na kurahisisha kufanyiwa  matengenezo  haraka iwezekanavyo.

Aliwashukuru wahisani  ambao wameunga mkono juhudi za Serikali katika kufanikisha mradi huo wakiwemo  Raas Alkheima, Viongozi mbali mbali  na wananchi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.