Habari za Punde

Hafla ya Uzinduzi wa Ripoti ya Kamisheni ya kimataifa, Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon,  akizungumza wakati wa uzinduzi wa Ripoti ya Kamisheni ya Kimataifa kuhusu“ Kizazi kinachojifunza: Uwekezaji  katika elimu   kwa dunia inayobadilika”. hafla ya uzinduzi wa  ripoti hiyo ambayo imeandaliwa na  Makamishna  27 akiwamo  Rais  Mstaafu wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete ilifanyika siku ya  jumapili  Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa.
  Rais mstaafu Kikwete akiwa na Makamishna wenzie kushoto ni  aliyekuwa  Kamishna wa Umoja wa  Ulaya Bw. Jose Manuel  Barroso na  Rais Mstaafu wa Mexico Bw. Felipe Calderon
 Sehemu ya washiriki wa hafla ya  uzinduzi wa Ripoti kuhusu Elimu
 Rais Mstaafu  Jakaya Kikwete akichangia na kuongoza majadiliano kuhusu kipengele cha ujumuishi katika elimu, ambapo  alisema ripoti hiyo imeainisha mikakati na mipango ya kuwafikia  makundi ya jamii yanayoishi katika mazingira magumu kama vile wakimbizi, wasichana, watoto wa mitaani, watoto walio katika ajira na watoto wanaobaguliwa.
 Kamishna Teopista Birungi  Mayanja kutoka  Uganda ambaye  katika mchango wake alisisitiza sana ushirikishwaji wa walimu katika mchakato mzima wa kuifanyia  mageuzi sekta ya elimu ili iweze kuwafikia watoto wote. akasisitiza pia umuhimu wa  walimu kuachwa watekeleze majukumu yao ya ualimu pasi ya kuingiliwa  au kuongezewa majukumu  nje ya  majukumu yao ya kufundisha
 Mwenyekiti wa Kamisheni na Mjumbe  Maalum wa Katibu Mkuu  kuhusu Elimu,   Waziri Mkuu Mstaafu wa Uingereza,Bw.  Gordon Brown akiwasilisha mbele ya  washiriki    taarifa  fupi ya  kilichomo kwenye ripoti ya kamisheni yake ambapo  suala kubwa   lililositizwa katika  ripoti hiyo ni uwekezaji wa raslimali fedha kwenye elimu. 
Rais   Mstaafu  Kikwete akisalimiana na Bibi. Ngozi Okonjo- Iwela Waziri wa zamani wa Fedha wa Nigeria

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.