Habari za Punde

Mahujaaj watakiwa kuwa mfano kwa matendo mema

Na Mwandishi wetu, Pemba

Waumini waliomaliza ibada ya hija nchini  wametakiwa kuwa mfano wa matendo mema yanayomridhisha Mwenyezi Mungu mbele ya jamii

Wito huo umetolewa na Al-haj ALI HAJI ALI huko katika Msikiti wa Istiqama Mkanjuni Chake chake alipokuwa akizungumza na Mahujaji  katika semina ya siku moja ya kutathmini safari ya Hija ya mwaka huu kupitia jumuiya  Al haramain Hajj Group

Alhaj Ali amesema ibada ya hija inamfanya Muumini kujifunza na kuelewa Ukubwa wa Mwenyezi Mungu na kuweza kuishi  kwa kumtii Yeye  na alivyoviumba katika mbingu na ardhi .

Aidha amewataka Mahujaji hao kuutumia uwezo walionao   kuwelimisha wengine kwenda kufanya hija ambayo ni lazima kwa kila  mwenye uwezo .

Akisoma risala katibu wa jumuiya hiyo Sheikh Hassan Rashid Mohamed ameeleza kusikitishwa na idadi ndogo ya mahujaji wanaojitokeza kwenda kuhiji.

Amesema bado safari ya hija hairidhishi kwa waislamu wa Zanzibar na kuwataka wenye uwezo kujitokeza kwa wingi kuiendea safari hiyo muhimu

Nao baadhi ya mahujaji waliokwenda hija kupitia jumuiya ya Al haramai wameipongeza jumuiya hiyo kwa kuboresha huduma zao kwa mahujaji wanaowahudumia.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.